Na Amina Kibwana,Glabu ya Jamii

  Muungano wa wapiga kura Tanzania (TANVU) umeandaa matembezi ya Hiayari ya upandaji mti kwa lengo la kuunga mkono  Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya Awamu ya tano.

  Matembezi hayo yanatarajiwa kuanza rasmi Novemba 26 hadi 30,2016, ambayo yataanzia Mkoani Singida wilaya ya Ikungi hadi Mkoa wa Dodoma ambapo zaidi ya wazalendo 600 wnatarajiwa kuhudhuria katika matembezi hayo.

  Akizungumza na waandishi wa habari Mratibu Msaidizi na Katibu mwenezi,Habari na Mawasiliano Barrynice Mayunga amesema kuwa katika matembezi hayo kutakuwa na upandaji wa miti ipatayo 12,500 (Elfu kumi na mbili na miatano)  kwa ajili ya utunzaji wa mazingira na misingi endelevu kwa viwanda.

  Amesema Mayunga, kwa kufanya hivyo pia itasaidia kujenga na kudumisha uzalendo ndani ya mioyo ya watanzania pamoja na kufanya kazi kwa kutumia kauli mbiu ya Rais Dkt John Pombe Magufuli wa Hapa kazi tu.

  "Sisi kama wazalendo tumeamua kujitoa kwa kufanya mate mbezi ya hiyari ili tuweze kukamilisha shughuli za upandaji miti kwa kuisaidia serikali ya awamu ya tano katika kuzisimamia rasilimali za nchi yetu."

  Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mipango na Uwezeshaji John Meena amesema kuwa miti ni pamoja na mikakati ya utunzaji wa mazingira kwani bila kuwa na miti kunaweza kusababisha madhara mbalimbali katika nchi ikiwemo, kuharibika kwa mifugo, kusababisha ukame nchini, Kupotea kwa mazao ya asili kama mbao,asali na matunda pamoja na kushuka kwa uzalishaji wa mazao na kuharibika kwa miundombinu ya hali ya hewa.
 
  Hata hivyo Muungano wa wapiga kura Tanzania (TANVU) umetoa wito kwa wanachi wote kujiandikisha na kuungana nao katika matembezi haya ili waweze kufikia lengo kwa pamoja kama wazalendo, Pia wameipomgeza serikali  yaawamu ya tano kwa jitihada inayoionesha katika kusimamia masuala mazima ya uwajibikaji kwa wanachi wake.
  Mratibu Msaidizi na Katibu mwenezi,Habari na Mawasiliano wa Muungano wa wapiga kura Tanzania Berrynice Mayunga akizungumza na waandishi wa habari, kulia ni Mshauri wa Muungano wa wapiga Kura Tanzania Mchungaji Donald Mathew.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...