Wafugaji wametakiwa kufuga kwa njia za kisasa kulingana na malisho badala ya kuwa na mifugo mingi huku wakikosa mahali pa kulishia.
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, William Tate Ole Nasha alipotembelea mnada uliopo mjini Mhunze wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.

Ole Nasha alisema si vyema wafugaji kuwa na mifugo mingi wakati hakuna rasilimali za kufugia kama nyasi ambazo katika maeneo mengi zipo chache hivyo kushindwa kukidhi mahitaji.Alisema pamoja na changamoto hizo Serikali kwa upande wake inaendelea na jitihada za kutatua changamoto hizo zinazowakabili wafugaji hapa nchini.

Aidha, Naibu waziri aliwataka wafanyabishara wa mifugo katika mnada wa Mhunze kujenga utamaduni wa kulipa ushuru wa Serikali badala ya kukwepa.Alisema kitengo cha kutorosha ng’ombe kukwepa kulipa ushuru wa mnada kunaikosesha Serikali mapato hivyo kushindwa kuwapa huduma.     
 Naibu Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, William Tate Ole Nasha (mwenye Kaunda suti ya bluu) akikagua ng’ombe ndani ya mnada wa Mhunze alipofanya ziara katika wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga.
 Naibu Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, William Tate Ole Nasha akizungumza na wananchi katika viwanja vya mnadani alipozuru mnada mji mdogo wa mhunzewilayani Kishapu.
 Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi akiwasikiliza wafugaji na wafanyabiashara wa mifugo katika mnada wa Mhunze.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...