PRIDE (Promotion of Rural Initiative and Development Enterprise)ni shirika lisilo la kiserikali (NGO) linalotoa huduma za kifedha kwa masharti nafuu kwa wafanyabiashara ndogondogo na wa kati. Huduma hizo zina lengo la kuchangia pato la taifa na kuondoa umasikini nchini. 

PRIDE ilisajiliwa mnamo Mei 1993 chini ya wadhamini wasio na hisa (Company Limited by guarantee, not Having Share Capital) kulingana na Sheria ya Makampuni Cap, 212 ya mwaka 2012.na kuanza rasmi shughuli zake mwaka 1994 mjini Arusha.Kwa sasa Shirika lina matawi 85 yalioenea nchi nzima.

Tangu kuanzishwa, PRIDE imeweza kukopesha wajasiliamali mbalimbali nchini wapatao 1,700,000 nakutoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni miatisa (bil. 900.0).

Katika kuungana naWatanzania, PRIDE Tanzania walitoa misaada mbalimbali moja kwa moja kwa wateja wao wa tawi la Bukoba ambao waliathirika na tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera.Msaada huu ulilenga kuwawezesha wateja wa PRIDE kukarabati makazi yao. 

Vilevile PRIDE ilichangia katika mfuko wa maafa wa serikali kwa kutoa mifuko ya saruji na mabati.
pr2
Mteja wa PRIDE Tanzania, tawi la Bukoba, Bw. Revocatus Siliden akionyesha madhara aliyoyapata kwenye nyumba yake baada ya kutokea tetemeko la ardhi huko Mkoani Kagera.
pr3
Afisa wa PRIDE Tanzania, Ndugu Samson Tenga akimkabidhi Mteja wa PRIDE Tanzania, Tawi la Bukoba mifuko ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa nyumba yake ambayo ilibomoka kutokana na janga la tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera.
pr4
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Mstaafu Salum Kijuu akifurahia jambo na mmoja wa wawakilishi wa wateja wa PRIDE Tanzania, tawi la BukobaBi. Mariam Seleman ambae pia ni muathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera.
pr5
Diwani wa Kata ya Miembeni, Manispaa ya Bukoba, Mkoa wa Kagera (Shati la Kijani) Bw. Richard Gaspar pamoja na maafisa wa PRIDE Tanzania wakimkabidhi mifuko ya saruji mteja wa PRIDE, ambaye nyumba yake iliathirika na tetemeko la ardhi lililotokea Bukoba.
pr6
Meneja wa Kanda ya Ziwa, Bi. Hilda Nsombo akikabidhi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Mstaafu SalumKijuu msaada wa mabati na mifuko ya saruji kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...