Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo leo amekutana na Bodi na Menejimenti ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), katika kikao kilichochadili maendeleo ya utekelezaji wa miradi inayosimamiwa na shirika hilo ikiwemo Mradi wa Kusindika Gesi Asilia, (LNG) na Mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Katika kikao hicho Prof. Muhongo ameitaka Bodi na Menejimenti hiyo kuongeza kasi katika utekelezaji wa miradi husika kutokana na manufaa ya miradi hiyo kwa Maendeleo ya Taifa.

Mbali na Bodi na Menejimenti ya TPDC, kikao hicho pia kimehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. Justin Ntalikwa, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia Madini, Prof. James Mdoe na baadhi ya Watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini.

Aidha, wakati huo huo, Waziri Muhongo pia amekutana na Balozi wa Uingereza nchini Sarah Cooke ambapo wamejadili masuala kadhaa kuhusu sekta ya nishati ikiwemo chanzo cha Nishati Jadidifu.Pia, Waziri Muhongo amekutana na Naibu Balozi wa Marekani nchini Virginia Blaser ambapo wamejadili masuala kadhaa kuhusu Sekta ya Nishati.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akisisitiza Jambo wakati wa Kikao chake na Bodi na Menejimenti ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).
Sehemu ya Menejimenti ya TPDC wakifuatilia kikao baina yao na Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo (hayupo pichani).
Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Uingereza nchini Sarah Cooke (wa pili kushoto) na ujumbe uliofuatana na Balozi huo.
Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo (katikati) akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini Sarah Cooken (wa kwanza kushoto) na ujumbe wake walipomtembelea leo ofisini kwake Jijijini Dar es Salaam. Kulia ni Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia umeme, Mhandisi Innocent Luoga.
Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo katika picha ya pamoja na Naibu Balozi wa Marekani nchini Virginia Blaser mara baada ya kumaliza mazungumzo yao wakati Naibu Balozi huyo alipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...