Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa Chad , Idriss Deby Itno baada ya Rais huyo kuwasili nchini Novemba 27, 2016. Katikati ni Makamu wa Rais Samia Suluhu. |
Rais
wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu leo tarehe 27 Novemba,
2016 majira ya jioni amewasili hapa nchini kwa ziara ya kiserikali ya
siku 3 kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli.
Katika
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es
Salaam, Rais Lungu amepokelewa na mwenyeji wake Rais Magufuli na
kulakiwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Mabalozi wanaowakilisha
nchi mbalimbali hapa nchini pamoja na wananchi.
Akiwa uwanjani hapo Rais Lungu amepokea heshima ya kupigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride rasmi lililoandaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
Akiwa uwanjani hapo Rais Lungu amepokea heshima ya kupigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride rasmi lililoandaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
Kesho
tarehe 28 Novemba, 2016 Rais Lungu ataendelea na ziara yake hapa nchini
ambapo pamoja na kutembelea miradi ya ushirikiano kati ya Tanzania na
Zambia ikiwemo TAZARA na TAZAMA, atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji
wake Rais John Pombe Magufuli, atashuhudia utiaji saini mikataba
mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Zambia na jioni
atahudhuria dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa na Rais Magufuli kwa ajili
yake Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Wakati
huo huo, Rais wa Jamhuri ya Chad Mhe. Idriss Deby Itno leo tarehe 27
Novemba, 2016 majira ya alasiri amewasili hapa nchini kwa ziara kikazi
ya siku 2.
Katika
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es
Salaam Rais Idriss Deby Itno akiwa na Mkewe Mama Hinda Deby amepokelewa
na mwenyeji wake Rais Magufuli na kisha kulakiwa na viongozi mbalimbali
wakiwemo Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe.
Kassim Majaliwa na wananchi.
Jioni hii, Rais Magufuli amefanya mazungumzo na Rais Idriss Deby Itno Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
27 Novemba, 2016
Jioni hii, Rais Magufuli amefanya mazungumzo na Rais Idriss Deby Itno Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
27 Novemba, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dkt John Pombe Magufuli akimtambulisha na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Chad Mhe Idriss Deby Itno kwa viongozi wa vikosi vya ulinzi na usalama mara baada ya kiongozi huyo kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jioni ya leo Novemba 27, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Chad Mhe Idriss Deby Itno mara baada ya kiongozi huyo kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jioni ya leo Novemba 27, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dkt John Pombe Magufuli akimzawadia kinyago cha Kimakonde cha "Umoja" na picha ya kuchora ya tembo na Mlima Kilimanjaro na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Chad Mhe Idriss Deby Itno mara baada ya kiongozi huyo kuwasili kwa mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam jioni ya leo Novemba 27, 2016
Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu akisalimiana na mabalozi wanaowakilisha nchi mbalimbali za Afrika nchini mara tu baada ya kupokewa na mwenyeji wake Rais Dkt John Magufuli katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jioni ya leo Novemba 27, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu wakisimama kwa ajili ya nyimbo za Taifa na mizinga 11 mara baada ya kiongozi huyo kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jioni ya leo Novemba 27, 2016Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu akikagua gwaride rasmi i mara tu baada ya kupokewa na mwenyeji wake Rais Dkt John Magufuli katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jioni ya leo Novemba 27, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dkt John Pombe Magufuli akimtambulisha Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu kwa Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe kassim Majaliwa baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jioni ya leo Novemba 27, 2016.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...