Nteghenjwa Hosseah – Arusha 

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Mashaka Gambo amekutana na kamati ya Amani ya Mkoa ambayo inajumuisha viongozi wa dini mbalimbali zilizoko katoka Mkoa huu kuzungumzia mustakabali wa Amani na namna viongozi hawa wa dini watashirikiana na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuleta maendeleo kwa wananchi ambao ni waumini wao.

Akizungumza katika Kikao hicho Mhe. Gambo alisema kazi ya Ulinzi wa Amani itakua rahisi sana kupitia viongozi wa dini ambao wana karama ya kuongea na kubadilisha maisha ya watu bila kutumia nguvu ama kuwashurutisha isipokua kwa chakula cha roho ambacho hujenga misingi imara ya imani na tabia njema.

Maendeleo ya wananchi hayawezi kupatikana bila Amani kuwepo katika Mkoa wetu ni lazima tusaidiane katika hili dhamira yetu ifanikiwe kwa wepesi zaidi tuna Imani kubwa sana Na viongozi wetu wa dini na ndio maana nikaona ni vyema tukakutana ili tusikie kutoka kwenu ninyi ambao mnawakilisha kundi kubwa la wananchi na pia kufahamu kero mbalimbali zinazowakwaza wananchi katika maeneo yenu alisema Gambo.
 
Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini Kati KKKT Solomon Masangwa akichangia kuhusu masuala yanayoweza kuhatarisha amani alisema kundi ambalo linatakiwa kuangaliwa kwa jicho la Tatu na litasaidia sana katika ulinzi wa Amani ni waendesha boda boda pamoja na wanachinga ambao kwa sasa wanaonekana kutopewa kipaumbele au hatuwajali kwa kiasi kinachostahili.

Tunapaswa kuangalia namna gani watu wanaofanya shughuli hizi wanakua rasmi kwa kupatiwa maeneo maalumu pamoja na utambulisho utakaowawezesha kufanya kazi zao kwa Amani na kujipatia kipato cha kuendesha maisha yao na si kama walivyo sasa wanafanya kazi hizo katika maeneo yasiyo rasmi na kuhama kila siku hali hii ina wafanya wajihisi kama si sehemu ya Taifa hili hivyo wanaweza kutumika kiurahisi kuhatarisha amani ya Nchi yetu alisema Masangwa.


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo(katikati) katika Picha ya pamoja na Viongozi wa Dini waliohudhuria Kikao cha Kamati ya Amani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...