Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amefanya ziara
wilayani Kishapu na kukagua mradi wa nyumba za watumishi wa Idara ya Afya zilizojengwa
kwa msaada wa Mfuko wa Benjamin William Mkapa.
Katika ziara hiyo Mhe. Telack akiwa ameambatana na Kamati ya
Ulinzi na Usalama ya Mkoa, alitembelea nyumba hizo katika kata za Shagihilu,
Mwakipoya na Idukilo ambazo tayari zimekamilika kwa ajili ya makazi.
Mkuu huyo wa mkoa aliiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
kuhakikisha kuwa changamoto zote zinazoikabili miradi hiyo na sekta ya afya kwa
ujumla zitatuliwe ziwe zimetatuliwa.
Aliitaka Idara ya Afya kushirikisha Idara ya Ujenzi katika
kutekeleza miradi inayohusu ujenzi wa mindombinu mbalimbali katika sekta hiyo
muhimu kwa kuwa ndiyo wataalamu.
Awali wakati akisoma taarifa ya halmashauri hiyo,
Mkurugenzi Mtendaji, Stephen Magoiga alisema jumla ya zahanati 22 zinajengwa na
Serikali kwa kushirikiana na wadau.
Magoiga aliongeza kwa kusema kuwa kukamilika kwa zahanati
hizo katika kata mbalimbali kutasaidia kutatua changamoto ya vifo vya
wajawazito na watoto.
Alibainisha kuwa hivi sasa halmashauri ina magari ya
wagonjwa (ambulance) manne ambapo matatu kati yake yalitolewa na Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNFPA) wakati moja lilinuliwa na halmashauri.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (mbele) akikagua
moja ya nyumba za watumishi wa Afya kata ya Shagihilu zilizojengwa kwa ufadhili
wa Mfuko wa Benjamin William Mkapa. Wengine pichani ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga (mwenye tai) na Mganga Mkuu
wa Mkoa, Mwita Ngutunyi (mwenye suti).
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga akiteta jambo na Mkurugenzi
Mtendaji mara baada ya kuwasili katika nyumba ya mtumishi wa Zahanati ya Kata
ya Idukilo wakati wa ziara yake wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa akifungua mlango wa moja ya nyumba
kujionea mradi huo uliofadhiliwa na Mfuko wa Benjamin William Mkapa wakati wa
ziara yake.
Mkuu wa Mkoa akiwasili katika zahanati ya Badi iliyopo
Kata ya Mwakipoya wilayani Kishapu kukagua miradi ya nyumba za watumishi wa
Afya. Wengine pichani kuanzia kushoto Afisa Mipango Wilaya, Mang’era Mang’era,
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya, Stephen Magoiga (mwenye tai) na
Mganga Mkuu wa Mkoa, Mwita Ngutunyi (mwenye suti).
Ukaguzi wa nyumba unaendelea huku Mhandisi Ujenzi
Wilaya, Samson Pamphil (kushoto) akichukua taarifa muhimu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...