Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati) akiongea wakati wa ufunguzi wa warsha kuhusu urithi wa Utamaduni Usioshikika inayoratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa wadau wa utamaduni leo Jijini Dar es Salaam. Wakwanza kushoto ni Mtaalam wa Utamaduni wa UNESCO Bi. Rehema Sudi anayefuatia ni Mtaalam wa Mipango kutoka UNESCO Bw. Mathias Luhanya na wakwanza kulia ni Mkufunzi wa Mafunzo hayo Bibi. Deirdre Solani.

Na Genofeva Matemu

Serikali imeahidi kuhifadhi kumbukumbu na takwimu sahihi za urithi wa Utamaduni usioshikika kwa lengo la kuuendeleza na kuiwezesha jamii kuulinda kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Rai hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel alipokua akifungua warsha ya siku kumi iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kuhusu urithi wa Utamaduni Usioshikika leo Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa warsha hiyo Prof. Gabriel amewataka washiriki kujifunza vizuri ili baadaye waweze kusaidia katika kuwekeza, kuibua, kutambua na kutunza urithi wa utamaduni ushioshikika kwani hiyo ndio njia mojawapo itakayowavutia watalii wengi kuja nchini kujifunza tamaduni zetu zisizoshikika.
Mtaalam wa Mipango kutoka UNESCO Bw. Mathias Luhanya (katikati) akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha kuhusu urithi wa Utamaduni Usioshikika kwa wadau wa utamaduni iliyoratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni(UNESCO) leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel na kushoto ni Mtaalam wa Utamaduni wa UNESCO Bi. Rehema Sudi.

“Utamaduni ni nta inayowaweka watu pamoja, ni vyema mafunzo haya na utaalamu mtakayoipata izingatie kuibua fursa na kutambua tamaduni ambazo hazishikiki kwani serikali ina malengo na matumaini makubwa sana kutoka kwenu” alisema Prof. Gabriel.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Utamaduni kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Lily Beleko amesema kuwa Tanzania iliweka saini na kuridhia mkataba wa kulinda urithi wa utamaduni usioshikika ambao ulipitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzanzaia mnamo mwaka 2011.

Anaongeza kuwa baadaye UNESCO kwa kushirikiana na Wizara inayohusika na mambo ya Utamaduni wamekua wakishirikiana katika kutoa mafunzo kwa wadau wa utamaduni na watu binafsi kuhusu namna ya kuhifadhi urithi wa utamaduni usishikika ambapo mafunzo hayo yanafanyika kwa mara ya nne sasa huku lengo likiwa ni kutekeleza mkataba huo.
Aidha Bibi. Beleko amesema kuwa watanzania wengi wamekua wakidhani kuwa utamaduni ushioshikika unahusiana na mambo ya kichawi hivyo kutotilia maanani umuhimu wake kitu ambacho si kweli kabisa kwa kuwa maana halisi ya utamaduni usioshikika unahusisha vitu vinavyohusiana na mazingira, maendeleo ya watu pamoja na mila na desturi zao yakiwemo maongezi, nyimbo, maigizo, midundo ndani ya ngoma ambayo yanaambatana na ala.

Naye Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bw. Mathias Luhanya amesema kuwa dhumuni la warsha ni pamoja na kuwajengea uwezo wadau wa utamaduni namna ya kuhifadhi urithi wa utamaduni usioshikika ili baadaye waweze kuorodhesha urithi huo kwani Tanzania ina bahati ya kuwa na jamii zaidi ya 120 hivyo ni matarajio kuwa urithi wa utamaduni usioshikika umesheheni ndani ya kila jamii.
Wadau wa Utamaduni wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi(hayupo katika picha) wakati wa ufunguzi wa warsha kuhusu urithi wa Utamaduni usioshikika leo Jijini Dar es Salaam. Picha na Lorietha Laurence.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...