Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said, akimtambulisha Mgeni wake Ndg Wilfred Moshi kwa Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe Zuberi Ali Maulid, alipofika kutembelea na kujionea shughuli za Baraza la Wawakilishi wakati wa Mkutano wake leo asubuhi.  
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Mtanzania wa Kwanza na Muafrika wa Tatu Duniani kupanda Mlima wa Evarest Ndg Wilfred Moshi alipofika katika jengo la Baraza la wawakilishi Zanzibar akiwa mgeni wa Mhe Simai Mohammed Said Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akimsikiliza Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said akitowa maelezo ya mgeni wake Ndg Wilfred Moshi ambae ni Mtanzania wa Kwanza kupanda Mlima Evarest.
Ndg Wilfred Moshi akitowa historia yake kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipofika katika majengo ya Baraza la Wawakilishi kwa mualiko wa Mhe. Simai Mohammed Said Mwakilishi wa Tunguu Zanzibar. akitowa historia yake ya kufanikiwa kupanda mlima huo mkubwa duniani na kuelezea tayari ameshapanda Mlima Kilimanjaro zaidi ya mara 100.  

Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.
Zanzinews.com.

HABARI  ZAIDI SOMA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...