Mwakilishi
wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said, akimtambulisha
Mgeni wake Ndg Wilfred Moshi kwa Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe
Zuberi Ali Maulid, alipofika kutembelea na kujionea shughuli za Baraza
la Wawakilishi wakati wa Mkutano wake leo asubuhi.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na
Mtanzania wa Kwanza na Muafrika wa Tatu Duniani kupanda Mlima wa Evarest
Ndg Wilfred Moshi alipofika katika jengo la Baraza la wawakilishi
Zanzibar akiwa mgeni wa Mhe Simai Mohammed Said Mwakilishi wa Jimbo la
Tunguu Zanzibar.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akimsikiliza
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said akitowa
maelezo ya mgeni wake Ndg Wilfred Moshi ambae ni Mtanzania wa Kwanza
kupanda Mlima Evarest..
Ndg
Wilfred Moshi akitowa historia yake kwa Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipofika katika majengo ya Baraza la
Wawakilishi kwa mualiko wa Mhe. Simai Mohammed Said Mwakilishi wa Tunguu
Zanzibar. akitowa historia yake ya kufanikiwa kupanda mlima huo mkubwa
duniani na kuelezea tayari ameshapanda Mlima Kilimanjaro zaidi ya mara
100.
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...