Mkurugenzi
Mkuu wa Bayport Financial Services, John Mbaga akikabidhi moja ya
kompyuta zilizokabidhiwa na Taasisi yake kwa ajili ya serikali.
Anayepokea ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Utawala Bora, Mheshimiwa Angellah Kairuki.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
TAASISI ya Kifedha ya Bayport Financial Services
inayojihusisha na mikopo imeipatia serikali msaada wa kompyuta 205 zenye
thamani ya Sh Milioni 500 kwa ajili ya matumizi yao ya kiofisi, kwa kupitia
Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Mkurugenzi
Mkuu wa Bayport Financial Services, John Mbaga wa pili kutoka kushoto
waliosimama, akipeana mkono na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala, Mheshimiwa Angellah Kairuki
baada ya kukabidhiwa kompyuta 205 na Taasisi ya Bayport, akifuatiwa na
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk Laurean Ndumbaro na Kaimu Katibu Mkuu Bi
Susan Mlawi.
Makabidhiano hayo yamefanyika jana jijini Dar es Salaam,
ambapo kompyuta 125 zitabaki Makao Makuu ya Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na kompyuta 80 zilizosalia zitagawanywa na
Wizara yenyewe kwa kuangalia mahitaji ya ofisi zao.
Baadhi
ya Wakuu wa Idara kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora wakifuatilia halfa ya makabidhiano ya kompyuta kutoka
kwa Taasisi ya Bayport Financial Services.
Akizungumza
katika makabidhiano hayo, Mkurugenzi Mkuu wa Bayport Financial
Services, John Mbaga, alisema msaada wa kompyuta hizo zinatokana na kiu
yao kubwa ya kushirikiana na serikali kuboresha utendaji kazi wa
watumishi wa umma kwa ajili ya kufanikisha huduma bora kwa Watanzania.
Alisema
taasisi yao ilipanga wamalize mwaka kwa kukabidhi kompyuta kwa ofisi za
serikali, ikiwa ni mwendelezo wa kusherehekea miaka 10 ya huduma zao
tangu Bayport ilipoanzishwa mwaka 2006 nchini Tanzania.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...