Na Eleuteri Mangi-MAELEZO, Dodoma.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametimiza siku ya 365 Watanzania wameona, kushuhudia utendaji na mwelekeo wake wa kuiongoza Serikali ya Awamu ya Tano kwa mafanikio.

Kauli hiyo imetolewa na leo Bungeni mjini Dodoma na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa kabla ya kuanza kujibu maswali ya papo kwa papo ambayo huulizwa na Wabunge kwa Waziri Mkuu kwa kumwomba Naibu Spika Dkt. Tulia Akson kuridhia kuwakumbusha Watanzania kuhusu muda wa uongozi tangu Rais Dkt. Magufuli aingie madarakani.

“Jukumu letu, ni kumwombea Mhe. Rais aweze kuendelea vizuri na kazi ya kuiongoza nchi yetu na wananchi wote tuungane pamoja kila moja kwa dhehebu lake kuweza kuiombea Serikali hii ili iweze kupata mafanikio makubwa” amesema Waziri Mkuu.

Akijibu swali lililoulizwa na Munde Tambwe Abdallah (Mb) juu ya mifumo ya Serikali ya kupeleka fedha za maendeleo katika halmashauri kwa kuzingatia mifumo, sheria, taratibu na miongozo ambayo husababisha halmashauri kuchelewa kupelekewa fedha mara baada ya bajeti kukamilika, Waziri Mkuu amesema kuwa baada ya Bunge la Bajeti kukamilisha kazi yake, Serikali inawajibika kutekeleza maamuzi ya Bunge kwa kupeleka fedha zilizopangwa kulingana na bajeti hiyo.

Akifafanua suala hilo, Waziri Mkuu amesema kuwa baada ya Bunge kuridhia na kutoa mamlaka ya matumizi ya fedha, Serikali ya Awamu ta Tano ilianza na majukumu muhimu ya kujiridhisha na uwepo wa mifumo sahihi ya makusanyo ya mapato na matumizi yake, kupeleka watumishi watakaosimamia shughuli za usimamizi wa ukusanyaji wa mapato na matumizi yake kwenye halmashauri zote nchini na kuratibu na kutathmini miradi yote iliyokuwa imeanza halafu kutokuendelezwa pamoja na miradi mipya ili kutambua pamoja na thamani zake.

Baada ya kujiridhisha juu ya mambo hayo, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali imeanza kupeleka kwenye halmashauri zote nchini ambapo kufikia mwezi Oktoba kwa mujibu wa Hazina, jumla ya zaidi ya shilingi Bilioni 177 za miradi ya maendeleo zimepelekwa kwenye halmashauri.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...