Katika kuadhimisha Siku ya Watoto Njiti duniani,Taasisi ya Doris Mollel inayojihusisha na maswala ya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati wameamua kuadhimisha siku hii kwa kumpelekea wheel chair, vyakula pamoja na box la sabuni kwa mama aliyejulikana kwa jina la Zainab Rashidi ambae ni mlemavu,mwenye watoto wawili waliozaliwa kabla ya wakati.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam,Msaidizi wa Kitengo cha Elimu-Taasisi ya Doris Mollel Rahma Amood amesema “Tumeamua kufanya hivi kwa lengo la kuhamasisha Taasisi nyingne na watu wengne waweze kuwakumbuka watoto hawa na kuweza kuwasaidia”. 

Doris Mollel Foundation kesho itaadhimisha siku hii kwa kutembea kilometa 3 visiwani Zanzibar kwa matembezi yatakayolenga kupunguza Watoto Njiti wanaozaliwa kote nchini. 

Kwa upande wake Mama huyo mwenye Watoto wawili waliozaliwa kabla ya wakati,Bi.Zainabu Rashid ameishukuru Taasisi hiyo kwa kumpa msaada huo kwa kumkumbuka.
Msaidizi wa Kitengo cha Elimu-Taasisi ya Doris Mollel, Rahma Amood akikabidhi msaawa wa wheel chair, vyakula pamoja na box la sabuni kwa mama aliyejulikana kwa jina la Zainab Rashidi leo jijini Dar es Salaam.
Msaidizi wa Kitengo cha Elimu-Taasisi ya Doris Mollel, Rahma Amood akimwelekeza, Zainab Rashidi njisi ya kutumia wheel chair leo jijini Dar es Salaam.
Msaidizi wa Kitengo cha Elimu-Taasisi ya Doris Mollel, Rahma Amood akiwa katika picha ya pamoja na Zainab Rashidi.
Msaidizi wa Kitengo cha Elimu-Taasisi ya Doris Mollel, Rahma Amood akiwa katika picha ya pamoja na familia ya Zainab Rashidi.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...