Washiriki wa Matembezi ya hisani ya kuadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Duniani yaliyotaribiwa na Taasisi ya Doris Mollel wakiwa na bango lenye ujumbe wa kuadhimisha siku hiyo, iliyoadhimishwa kitaifa Mjini Unguja, Zanzibar Novemba 19, 2016. Matembezi hayo yalianzia katika Uwanja wa Amani kupitia Uwanja wa Tumbaku na kuishia Viwanja vya Maisara.
 Baadhi ya viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakijumuika pamoja Wadhamini na Waratibu wa Matembezi ya hisani ya kuadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Duniani, wakishiriki Matembezi hayo, yalianzia katika Uwanja wa Amani kupitia Uwanja wa Tumbaku na kuishia Viwanja vya Maisara, Mjini Unguja, Zanzibar.
Brass Band ya Chuo cha Mafunzo, Zanzibar ikiongoza Matembezi ya hisani ya kuadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Dunian,  iliyoadhimishwa kitaifa Mjini Unguja, Zanzibar Novemba 19, 2016. Matembezi hayo yalianzia katika Uwanja wa Amani kupitia Uwanja wa Tumbaku na kuishia Viwanja vya Maisara.
Mkuu wa Kitengo ya Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Jacqueline Materu akiwa pamoja na Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris Mollel pamoja na washiriki wengine katika Matembezi ya hisani ya kuadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Duniani, yaliyoadhimishwa kitaifa Mjini Unguja, Zanzibar Novemba 19, 2016.
Mgeni Rasmi katika hafla ya Matembezi ya hisani ya kuadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Duniani, Naibu Waziri wa Afya Zanzibar, Harusi Said Suleiman  aliemuwakilisha Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mama Asha Balozi, akitoa hotuba yake, katika hafla ya Kilele cha siku ya Mtoto Njiti Duniani, iliyoadhimishwa kitaifa Mjini Unguja, Zanzibar Novemba 19, 2016. Vodacom ndio Wadhamini wakuu walioeza kufanyikisha shughuli hiyo. Kulia ni Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel na Mratibu wa Matembezi hayo, Doris Mollel na kushoto ni Mkuu wa Kitengo ya Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Jacqueline Materu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...