Unapowadia mwisho wa mwaka wizi kupitia mtandao umekua ukishika kasi zaidi. Mataifa mengi duniani yamekuwa yakikumbwa na wimbi kubwa la uhalifu mtandao unaoambatana na upoteaji wa pesa. Itakumbukwa mwaka jana kuelekea mwisho wa mwaka ndio kirusi kipya aina ya ModPOS kilionekana kwa mara ya kwanza na kilifanikiwa kudhuru maeneo mengi na kusababisha kiasi kikubwa cha fedha kupotelea mikononi mwa wahalifu. 


Mwezi huu wa Novemba  pekee tayari kumekua na matukio mengi yenye mlengo wa kuwapatia pesa wahalifu mtandao. Kwa sasa Uhalifu mtandao kpitia kirusi cha RANSOMWARE kinachoendelea kushikakasi wamefanikiwa kupata mamilioni ya fedha. Kirusi hiki kinapelekea mhalifu mtandao kumfungia uwezo mmiliki halali kutumia kifaa chake akimtaka alipe kiasi cha pesa ili kurudishiwa huduma. Uhalifu huu umepiga hodi Barani Afrika na hadi sasa wengi wameendelea kuathirika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...