Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

SHIRIKISHO la mpira wa miguu  nchini TFF,limepokea mwaliko kutoka chama cha mpira wa miguu nchini Zimbabwe juu ya chama hicho kuhitaji kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa na timu ya Tanzania Taifa Stars.

Afisa habari wa TFF,Alfred Lucas amesema kwamba mara baada ya kupokea baraua hiyo shirikisho la soka hapa nchini limeridhia swala hilo na kwa sasa wakati wowote kuanzia sasa kocha mkuu wa timu ya Taifa Chars Boniphace Mkwasa ataanza program kwa ajili ya mechi hiyo inayotaraji kupigwa siku ya tarehe 13 mwezi huu.

 Kocha Mkwasa anatarajiwa kutangaza kikosi hivi karibuni na wataingia kambini kwa ajili ya kujiandaa na mechi hiyo ambayo ni muhimu sana kwao kwa ajili ya kupanda viwango vya FIFA.

Awali timu hiyo ilitakiwa kucheza na Ethiopia katika kalenda ya FIFA ila iliweza kufutwa kutokana na hali ya usalama kuwa mbaya nchini humo.

Kwa sasa Tanzania imeshuka katila viwango vya FIFA na kufika nafasi ya 142 kidunia.                        

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...