Na Genofeva Matemu - WHSUM.

Serikali ya Tanzania itaendelea kuweka historia ya Ukombozi wa Bara la Afrika kwa kuhifadhi kumbukumbu zote huku ikitunza na kuweka alama maeneo ambayo yalitumika wakati wa kupigania Uhuru wa Bara la Afrika na kutunza makaburi ya wapigania uhuru hao pamoja na kuyafanya kuwa ya kihistoria.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipokutana na Waziri wa Utamaduni na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe.Nathi Mthehwa aliyeko nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa nchi hizo mbili katika sekta ya Utamaduni na Sanaa.

 “Tumeanza kuandika historia ya Ukombozi wa Bara la Afrika kwa kuhoji baadhi ya wanaharakati walioshiriki katika kuwasaidia wapigania uhuru kuanzisha vyama vyao vya ukombozi ambapo historia hii itahifadhiwa kwa njia ya sauti na picha lakini pia tutaendelea kutunza kumbukumbu zote tutakazozipata na kuwekea alama maeneo ambayo yalitumika wakati wa kupigania uhuru” amesema Mhe. Nnauye

Aidha, Mhe. Nnauye amesema kuwa makubaliano yaliyosainiwa mwaka 2011 kati ya Tanzania na Afrika ya Kusini kufuta Visa ya kusafiria kati ya nchi hizo mbili yameleta  mabadiliko makubwa katika eneo la Sanaa nchini kwani wasanii wamekua wakitumia fursa hiyo kwenda Afrika ya Kusini kuandaa kazi zao na kuzifanya kuwa na ubora zaidi.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye (kulia) akieleza jambo kwa Waziri wa Sanaa na Utamaduni wa   Afrika ya Kusini Ndg. Nathi Mthehwa(kushoto) ambaye yupo nchini kwa ziara ya kikazi kwa siku tatu yenye lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo kupitia Sanaa na Utamaduni ikiwemo kuhifadhi historia ya ukombozi wa Afrika ya Kusini leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel (kulia) akisalimiana na Waziri wa Sanaa na Utamaduni wa Afrika ya Kusini Ndg.Nathi Mthehwa (Kushoto) leo Jijini Dar es Salaam alipotembelea Wizara hiyo kwa ajili ya mazungumzo ya kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizo katika sekta za Sanaa na Utamaduni, katikati ni Balozi wa Afrika ya Kusini Nchini  Thamsanga Dennis Mseleku.
Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye  akiongea na waandishi wa habari (hawapo katika Picha) leo Jijini Dar es Salaam kuhusu ziara ya Waziri wa Sanaa na Utamaduni wa Afrika ya Kusini Ndg. Nathi Mthehwa  ambaye yupo nchini kwa siku tatu kwa lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo kupitia sekta ya Sanaa na Utamaduni ikiwemo kuhifadhi historia ya ukombozi wa Afrika ya Kusini.
Waziri wa Sanaa na Utamaduni wa   Afrika ya Kusini Ndg. Nathi Mthehwa (kulia) akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu ziara yake ya siku tatu nchini leo Jijini Dar es Salaam (kushoto) ni Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye . 
Mshauri Mtaalamu wa Urithi wa Utamaduni Dkt.Daniel Ndagala akichangia hoja  wakati wa kikao baina ya Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye na Waziri wa Sanaa na Utamaduni wa   Afrika ya Kusini Ndg. Nathi Mthehwa leo Jijini Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...