Mtandao wa asasi za kiraia unaojihusisha na masuala ya Maji na mazingira Nchini (TaWaSaNet) umeandaa mkutano  uliowakutanisha wadau Mbalimbali wa Mazingira Nchini, ili kuadhimisha  wiki ya usafi wa Mazingira inayoenda sambamba na siku ya choo na kunawa mikono Duniani inayo adhimishwa novemba 19 ya kila mwaka.

Akizungumza katika mkutano huo mgeni rasmi Naibu waziri wa Afya Jinsia wazee na Watoto Dkt Khamisi Kigwangala amesema, wizara yake imejipanga kusimamia kwa ukaribu  utekelezaji wa mikakati mbalimbali ya  kitaifa na kimataifa inayolenga upatikanaji wa vyoo bora mashuleni na kwenye vituo vya Afya.

Dkt Kigwangala ameipongeza Taasisi ya TaWaSaNet kwa kufanikisha na kuandaa mkutano huo kwa kuwa wadau wazuri wa mazingira na kuzitaka asasi nyingine za kiraia kuunga mkono jitihada za serikali ya Awamu ya Tano katika kuendeleza kampeni mbalimbali za usafi  hapa Nchini.

Katika mkutano huo Kigwangala ametoa Tuzo kwa wanahabari mahiri kwenye uandishi wa makala usafi na mazingira ambapo  Bw.Gervas Hubile amepata tuzo ya makala bora ya usafi wa mazingira kwa upande wa radio na Bi Salome Gregory ametwaa tuzo ya Makala bora ya usafi wa mazingira kwa upande wa magazeti.

 Naibu waziri wa Afya Jinsia wazee na Watoto Dkt Khamisi Kigwangala akizungumza na wadau mbalimbali wa mazingira juu ya kutoa tuzo kwa wanahabari mahiri kwenye uandishi wa makala usafi na mazingira leo jijini Dar es Salaam.  
 .Afisa Sera wa Taasisi ya Tanzania Water and Sanitation Network (TAWASANET), Darius Mhawi wa (kwanza kushoto) akizungumza machache  kwenye utoaji wa tuzo kwa wanahabari mahiri kwenye uandishi wa makala usafi na mazingira leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu waziri wa Afya Jinsia wazee na Watoto Dkt Khamisi Kigwangala akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali  leo jijini Dar es Salaam.picha na Yasir Adam wa Globu ya jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...