BENDI ya muziki wa taarabu ‘Yah TMK Morden Taarab’ inafaya utambulisho wa nyimbo zake mbili za mwanzo, utakaofanyika Alhamis ya Novemba 10 mwaka huu.

Akizungumzia na mtandao huu, Mkurugenzi wa bendi hiyo Said Fella, alisema kuwa utambulisho huo maalum utaanza katika vyombo vya habari kwa kuanza kupiga nyimbo hizo katika vituo vya hapa nchini.

Alisema nyimbo mbili zilizomaliza kurekodiwa ambazo zimeimbwa na wanamuzi mahili ambao ni Mwanahawa Ali aliyeimba wimbo wa Sina Puma na Aisha Vuvuzela aliyeimba wimbo wa ‘Kibaya kina Wenyewe’ .

Fella alisema bendi hiyo inayoundwa na wanamuziki mahili wa muziki huo , Mussa Mauji, Mussa Mipango, Omar Tego, Fatuma Nyoro, Mauwa Tego, Babu Kijiko na wengine waliopo kwenye bendi hiyo wanatoka kwenye kituo cha Mkubwa na wanawe ni pamoja na Mwanadada Jeza, pamoja na Hassan Dogo na Ibrahim.

Alisema kuwa hata hivyo wataendelea kurekodi nyimbo nyingine na kuzitambulisha kama mwendelezo mpaka kufika uzinduzi wa albamu na bendi yao hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...