Na Amina Kibwana,Globu ya Jamii
Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kwa kushirikiana na Ubalozi wa china
hapa nchini ,imeandaa semina kwa ajili ya jumuiya ya wafanyabiashara wa
China kwa lengo la kuwaelimisha juu ya masuala mbalimbali ya ulipaji
kodi.
Semina hiyo inayotarajiwa kufanyika Novemba 25 katika ukumbi wa Benki kuu ya Tanzania (BoT), inatarajiwa
kufunguliwa na Waziri wa Biashara na viwanda Mh. Charles Mwijage pamojana na Balozi wa China hapa nchini.
Ikiwa ni semina ya 15 tangu kuanza kwa
semina kati ya mamlaka ya Mapato Tanzania na Ubalozi wa china,TRA imekuwa
ikiendesha semina mbalimbali kwa wachina kuhusu masuala ya kodi kwa
maombi au kutokana na mipango ya TRA kuelimisha makundi mbalimbali ya
walipa kodi ili kuongeza uelewa wa Masuala ya Kodi hapa nchini.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi kutoka TRA Richard Kayombo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu semina kwa jumuiya ya wafanyabiashara wa china itakayofanyika tarehe 25 Novemba 2016, leo jijini Dar es Salaam.Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Jiteng Consultancy Limited Bw. Andrew Huong na Meneja Msaidizi wa Kampuni hiyo Bw. Wesley Huung (kushoto). Picha na Frank Shija – MAELEZO.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...