Na Adili Mhina, Kigoma
Wizara ya Fedha na Mipango -Tume ya Mipango kwa kushirikiana na Serikali ya Ubelgiji inaendesha mafunzo ya maandalizi ya miradi ya maendeleo kwa ajili ya ufadhili wa washirika wa maendeleo kwa Mkoa wa kigoma.

Akifungua mafunzo hayo yanayoendelea mjini kigoma na kuwashirikisha Makatibu Tawala, Wakurugenzi na wataalam wa sera na mipango kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa kigoma, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Bibi Florence Mwanri alieleza kuwa Serikali ya Ubelgiji ambayo ndio iliyofadhili mafunzo hayo kuwa imefanya jitihada kubwa katika kufadhili miradi mbalimbali katika Mkoa wa Kigoma.

“Tunaishukuru sana Serikali ya Ubelgiji kwani kwa kipindi kirefu imekuwa ikifanya kazi kubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo hususan kwenye sekta za kilimo na maji ambapo kwa kiwango kikubwa imesaidia kuboresha maisha ya wananchi wa mkoa huu,” alieleza Bibi Mwanri.

Alisisitiza kuwa licha ya mafanikio yaliyopatikana kupitia miradi iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa na Serikali ya Ubelgiji katika Mkoa wa Kigoma zipo changamoto kadhaa ambazo zimeonekana kupunguza ufanisi wa miradi husika.

Miongoni mwa changamoto hizo ni; rushwa, kiwango kisichoridhisha cha uratibu wa utekelezaji wa miradi, uwakilishi duni katika kamati za utekelezaji wa miradi na ugumu wa kupata taarifa za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Changamoto nyingine ni pamoja na miundombinu mibovu hususan barabara na umeme ambayo inachangia kutokuvutia wataalam kuishi katika mkoa wa Kigoma, na uhaba wa utaalam katika maandalizi, kutekeleza na kusimamia kwa ufanisi fedha zinazotumika kugharamia miradi ya maendeleo.

Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Florence Mwanri akitoa hotuba ya Ufunguzi wa mafunzo ya miradi ya maendeleo kwa ajili ya ufadhili wa washirika wa maendeleo kwa Mkoa wa kigoma. Kulia ni mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa kigoma Bw. Samwel Tenga, wa kwanza kushoto ni Kaimu Naibu Katibu Mtendaji Klasta ya Uchumi Jumla kutoka Tume ya Mipango, Dkt. Lorah Madete na pembeni yake (mwenye tai) ni Mratibu wa mafunzo hayo Bw. Paul Sangawe.


Mratibu wa Mafunzo Bw. Paul Sangawe akitoa maelezo juu ya utayari wa washirika wa maendeleo katika kufadhili miradi ya maendeleo nchini. Kulia ni Kaimu Katibu Mtendaji Tume ya Mipango Bibi Florence Mwanri na Kushoto ni Dkt. Lorah Madete kutoka Tume ya Mipango.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ambao ni Makatibu Tawala, Wakurugenzi na wataalam wa sera na mipango kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Kigoma wakiendelea wakifuatilia mafunzo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...