Kamanda wa jeshi la polisi kanda maalumu mkoa wa Dar es salaa,Saimon Siro
Na Anthony John,Globu ya Jamii
Kamanda wa jeshi la polisi kanda maalumu mkoa wa Dar es salaa,Saimon Siro amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuweza kuwabaini wauzaji wa madawa ya kulevya aina hiyo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salam Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamishna Simon Sirro amesema zoezi hilo bado linaendelea ili kuwabaini wauzaji wa shisha.
Amesema katika Wilaya ya Kinondoni wamefanikiwa kuwakamata watu watatu na vielelezo,amesema watawapeleka mahakamani baada ya kupeleka vielelezo kwa Mkemia Mkuu wa serikali na taratibu za mahakamani zitaendelea.
‘’Opareshini dhidi ya shisha bado unaendelea na tunawaomba wananchi wa mkoa wa Dar es salaam waendelee kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili tuweze kuwabaini wauzaji wa dawa za kulevya aina ya shisha’’ amesema Kamanda Sirro
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...