Jumla ya vijana 50 wameondoka nchini leo kuelekea China, kusomea
kozi mbalimbali ikiwemo za afya na uhandisi katika masuala ya Petroli kwa ngazi
ya Shahada ya Kwanza masomo yatakayochukua miaka minne na sita kutegemea na
aina ya kozi.
Wakizungumza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere
jijini Dar es Salaam, muda mfupi kabla ya kupaa kuelekea China, vijana hao
wameelezea matumaini yao kuwa stadi na maarifa wanakayokwenda kupata nchini
humo katika Shahada za Udaktari na Upasuaji, Uhandisi wa Masuala ya Petroli na
Usanifu Majengo, vitakuwa na tija kwao na taifa kwa ujumla.
Thomas Macha na Sabir Abdulrahman, wanaokwenda katika vyuo vikuu
vya majimbo ya Shenyang na Hubei, wamezungumzia matarajio yao, wakiamini
masomo wanayoenda kusoma yataisaidia Serikali kuelekea Tanzania ya Viwanda
inayohubiriwa na Serikali ya Wamu ya Tano.
Miongoni mwa wasichana 20 kati ya vijana hao 50 wanaokwenda nchini
humo, Monica Malugu na Anastacia Meresho, nao wamezunguzia matarajio yao
ikiwemo mitazamo kuwa wanawake hawawezi masomo fulani kwa kuwa ni magumu.
Aidha, Glory Minja, mwakilisi wa Taasisi ya Universal Abroad Link (UAL), yenye dhamana ya kuwatafutia vyuo na ushauri kulingana na soko la ajira na kujiajiri, amesema,kila kitu kiko sawa na kwamba wanasubiriwa kuanza masomo.
Aidha, Glory Minja, mwakilisi wa Taasisi ya Universal Abroad Link (UAL), yenye dhamana ya kuwatafutia vyuo na ushauri kulingana na soko la ajira na kujiajiri, amesema,kila kitu kiko sawa na kwamba wanasubiriwa kuanza masomo.
Meneja wa Taasisi ya Universities Abroad Link (UAL), Joash Hosea akiagana na baadhi ya wanafunzi wanaokwenda kusoma katika vyuo vikuu vya nchini China kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Jumla ya wanafunzi 50 wamekwenda China kwa ajili ya masomo ya Udaktari, Uhandisi pamoja na Mafuta na Gesi.
Baadhi ya wanafunzi wanaokwenda kusoma katika vyuo vikuu vya nchini China wakimsikiliza Meneja wa Taasisi ya Universities Abroad Link, Joash Hosea kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana. Jumla ya wanafunzi 50 walikwenda China kwa ajili ya masomo ya Udaktari, Uhandisi pamoja na Mafuta na Gesi. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...