Na Eliphace Marwa - Maelezo

Ni mwaka mmoja tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani na kutekeleza kwa vitendo moja ya ahadi alizozitoa Mgombea Urais wakati ule, Dkt. John Pombe Magufuli ya kuanzisha Mahakama ya Rushwa na Mafisadi.
 

Mahakama ambayo imeanza miezi michache iliyopita inaleta matumaini kwa watanzania hasa wanaipenda nchi yao wakiwa na uzalendo na fikira za kiutaifa. Katika ahadi za TANU, baadae CCM imetamkwa wazi kuwa Rushwa ni adui wa Haki, Sitapokea wala Kutoa Rushwa.

Rais John Pombe Magufuli anatekeleza kwa vitendo anachokiahidi. Leo naomba nizungumzie utekelezaji wa ahadi yake ya kuanzishwa kwa mahakama maalum ya kushughulikia mafisadi na wahujumu uchumi wa nchi yetu.

Ni dhahiri kuwa Dkt. Magufuli anafuata nyayo za muasisi wa Taifa letu, Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alithubutu kukemea na kuwaadhibu viongozi wote wala rushwa.

Mwalimu Nyerere alichukia sana rushwa na alichukua hatua kali sana kwawala rushwa wote bila kujali nyadhifa zao au uwezo wao wa kifedha kwani nakumbuka kuna waziri wake mmoja alihukumiwa kifungo na viboko baada ya kupatikana na hatia ya kula rushwa .

Watumishi wa umma, waliohusika na ufisadi walichukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kufungwa jela na kufilisiwa mali zao na hiyo ilipunguza sana rushwa na ifisadi serikalini. Mwalimu aliamini kwamba mtu hawezi kupanda farasi wawili kwa wakati mmoja na alikuwa sahihi kabisa. Kitendo cha kuruhusu wafanyabiashara kuingia kwenye siasa, na viongozi kuruhusiwa kufanya biashara ndio chanzo cha wizi na ufisadi wa mali na fedha za umma.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...