Umoja
wa Mataifa umeingia ushirikiano na FURSA ili kuongeza uelewa wa malengo
ya maendeleo endelevu kwa vijana zaidi ya 10,000 katika mikoa mitatu ya
Dodoma, Dar es Salaam pamoja na Kigoma.
Fursa,
ambayo imekuwa ikifanyika kwa miaka mitatu iliyopita, imejikita katika
kuwajengea uwezo vijana wa kuzitambua fursa katika maeneo yao wanayoishi
lakini pia namna ya kutengeneza miradi na biashara kupitia fursa hizo.
Ushirikiano
wa Fursa na Umoja wa Mataifa utalenga kuwafikia vijana wanaohudhuria
semina za Fursa kuelewa namna Malengo ya Dunia yanavyohusiana na maisha
yao ya kila siku na wajibu wa kila kijana katika kushiriki
kuyakamilisha.
Akizungumza
wakati wa kuzindua semina za Fursa mkoani Dodoma, Mratibu Mkazi wa
Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez alisema semina za Fursa zimeweza
kubadilisha maisha ya vijana wengi na hivyo ushirikiano wake na Umoja wa
Mataifa katika kufikia vijana utatoa nafasi ya vijana kuyaelewa Malengo
ya Dunia.
‘Vijana
wengi wana ari ya kushiriki katika kufanikisha Malengo ya Dunia, ndio
maana Umoja wa Mataifa umeamua kushirikiana na Fursa ili kuhakikisha
vijana wengi zaidi wanayafahamu malengo haya lakini pia wanashiriki
katika kuyatekeleza’ alisema Alvaro.
Kwa
upande wake, Mwanzilishi wa Fursa, Ruge Mutahaba amesema kwa zaidi ya
miaka mitatu sasa Fursa imefanikiwa kuwafikia zaidi ya vijana milioni 5,
na kuwapa mbinu na maarifa ya kuweza kutumia fursa katika maeneo yao.
‘Tunaushukuru
Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na Fursa kuwafikia vijana katika
mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam na Kigoma, ili sio tu wapate nafasi ya
kupata mafunzo ya Fursa na biashara balipia mafunzo juu ya Malengo ya
Dunia’ alisema Ruge.
Timu ya wazungumzaji wa Fursa wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi waShirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa, Hoyce Temu.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi waShirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akizungumza na vijana waliohudhuria semina ya Fursa mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki hii.
Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu akitoa mafunzo ya malengo ya maendeleo enedelevu kwa vijana wa Dodoma waliojitokeza wakati wa semina za Fursa zilizofanyika Dodoma mwishoni mwa wiki hii.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi waShirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi mmoja wa vijana waliopata mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa mjini Dodoma. Anayetazama kushoto ni Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu.
Baadhi ya vijana waliopata mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa mjini Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi waShirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akizungumza na vijana waliohudhuria semina ya Fursa mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki hii.
Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu akitoa mafunzo ya malengo ya maendeleo enedelevu kwa vijana wa Dodoma waliojitokeza wakati wa semina za Fursa zilizofanyika Dodoma mwishoni mwa wiki hii.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi waShirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi mmoja wa vijana waliopata mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa mjini Dodoma. Anayetazama kushoto ni Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu.
Baadhi ya vijana waliopata mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa mjini Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...