Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
MWANDAMIZI wa masuala ya usalama barabarani , Lawrence Kilimwiko amewataka waandishi wa habari  kutumia kalamu zao kuelimisha umma juu ya usalama bora na namna ya kukabiliana nazo.

Akitolea ufafanuzi juu ya masuala ya usalama barabarani, Kilimwiko amesema kuwa waandishi wengi wa habari wanaripoti habari za ajali kama matukio na kushindwa kufuatilia hasa baada ya kumaliza kuandika hawafanyi ufuatiliaji wa majeruhi.

Kilimwiko amesema kwa ajali za barabarani zimekuwa janga la afya hasa baada ya takribani watu milioni 50 wanaathirika na ajali hizo na wengine kupoteza maisha  na kundi kubwa linaloathirika ni vijana na inakadiriwa kufika mwaka 2030 ajali za barabarani zitachukua namba 5 katika janga la vifo duniani.

Kutokana na ajali hizo, zimesababisha kupeleka mzigo mkubwa kwa sekta ya afya na kupelekea kuongeza gharama za serikali na kuchangia umasikini kutokana na nguvumali ya taifa kuangamiakwa ajali za barabarani.

Uchunguzi uliofanyika kupitia Shirika la Afya Duniani(WHO) kupitai usalam barabarani  wamegundua kuwa asilimia 95 za  ajali zinatokana na matumizi mabya ya barabara na kuhamasisha waandishi wa habari kusaidia na kuchochea mabadiliko ya sera za sheria za Usalama barabarani.

Kilimwiko amesema nchi kama Afrika Kusini ina sheria ambayo dereva yoyote haruhusiwi kutumia simu wakati anaendesha chombo cha moto na atakapokamatwa basi atapigwa faini na hili linatakiwa kufanyika hata nchini kwetu na hilo litasaidia kupunguza ajali.
 Mwandamizi wa masuala ya Usalama Barabarani, Lawrence Kilimwiko akizungumza na waandishi wa habari juu ya masuala ya Usalama barabarani na jinsi ya kuelimisha jamii kuhusiana na sera za usalama bwa barabara katika semina elekezi kutoka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA).
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa makini kumsikiliza mwandamizi wa masuala ya usalama barabarani Lawrence Kilimwiko.Picha na Zainab Nyamka,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...