Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisaini Maazimio ya Wabunge wa Tanzania yenye dhamira ya kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu" TB Caucus ",mtandao huo ulianzishwa jijini Barcelona,Hispania Oktoba 2014 na kuitwa Mtandao wa Wabunge duniani "The Global TB Caucus
Mjumbe wa Mtandao wa wabunge duniani,Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akisaini maazimio hayo
Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii, Mhe. Peter Serukamba akisaini maazimio hayo ya wabunge wa Tanzania.nchini Tanzania takribani wagonjwa 160,000 huugua kifua kikuu kila mwaka.
Naibu Mratibu wa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua kikuu na ukoma Dkt. Liberate Mleoh akijibu maswali yaliyoulizwa na waheshimiwa wabunge wakati wa semina ya wabunge kuhusu kifua kikuu iliyofanyika kwenye ukumbi wa wabunge jijini Dodoma.
Afisa mpango toka mpango wa taifa wa kudhibiti kifua kikuu na ukoma Dkt. Deus Kamala akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wabunge.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...