Na K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewataka wadau wa umeme kujadili maombi ya Shirika la Umeme Nchini TANESCO ya kupandisha bei ya umeme kwa asilimia 18.9 kwa uwazi na bila hofu lakini wakizingatia nia ya Serikali ya awamu ya tano ya kujenga nchi yenye uchumi wa viwanda.

Akifungua majadiliano ya wadau wa Mkoa wa Dar es Salaam, Zanzibar na uongozi wa TANESCO jijini Novemba 23, 2016 kwenye ukumbi wa mikutano wa Mamlaka ya Udhibiti Huduma za Maji na Nishati, (EWURA), kuhusu mapendekezo hayo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi, (pichani juu), ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa, Paul Makodna alisema, “Rais wetu Mh. Dkt. John Pombe Magufuli, amedhamiria kujenga uchumi wa viwanda ambao utafanikiwa tu endapo tutakuwa na umeme wa uhakika na ulio bora.” Alisema.
 Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Umeme nchini TANESCO, Mhandisi Decklan Mhaiki, akiwasilisha mambi ya shirika hilo ya kupaandishi bei ya umeme kwa asilimia 18.9 wakati wa kikao cha majadiliano baina ya wadau na uongozi wa shirika, kilichoitishwa na Mamlaka ya Udhibiti huduma za Maji na Nishati, (EWURA), na kufanyika jijini Dar es Salaam, Novemba 23, 2016.
 Baadhi ya viongozi wa TANESCO na wadau wakifuatilia mjadala

Aliwataka wadau kusikiliza kwa makini hoja za TANESCO zinazowasukuma kupandisha bei ya umeme, lakini TANESCO nao wanapaswa kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu mapendekezo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...