Na
K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
MKUU
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewataka wadau wa umeme kujadili
maombi ya Shirika la Umeme Nchini TANESCO ya kupandisha bei ya umeme kwa
asilimia 18.9 kwa uwazi na bila hofu lakini wakizingatia nia ya Serikali ya
awamu ya tano ya kujenga nchi yenye uchumi wa viwanda.
Akifungua
majadiliano ya wadau wa Mkoa wa Dar es Salaam, Zanzibar na uongozi wa TANESCO jijini Novemba 23, 2016
kwenye ukumbi wa mikutano wa Mamlaka ya Udhibiti Huduma za Maji na Nishati,
(EWURA), kuhusu mapendekezo hayo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi,
(pichani juu), ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa, Paul Makodna alisema, “Rais wetu Mh. Dkt.
John Pombe Magufuli, amedhamiria kujenga uchumi wa viwanda ambao utafanikiwa tu
endapo tutakuwa na umeme wa uhakika na ulio bora.” Alisema.
Kaimu
Mkurugenzi wa Shirika la Umeme nchini TANESCO, Mhandisi Decklan Mhaiki,
akiwasilisha mambi ya shirika hilo ya kupaandishi bei ya umeme kwa
asilimia 18.9 wakati wa kikao cha majadiliano baina ya wadau na uongozi
wa shirika, kilichoitishwa na Mamlaka ya Udhibiti huduma za Maji na
Nishati, (EWURA), na kufanyika jijini Dar es Salaam, Novemba 23, 2016.
Baadhi ya viongozi wa TANESCO na wadau wakifuatilia mjadala
Aliwataka
wadau kusikiliza kwa makini hoja za TANESCO zinazowasukuma kupandisha bei ya
umeme, lakini TANESCO nao wanapaswa kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu
mapendekezo yao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...