Mkurugenzi Muendeshaji wa Kiwanda cha kutengeneza vifungashio cha Global Packaging Limited Bw. Joseph Wasonga na wafanyakazi wa kiwanda wakimtembeza Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt.Adelhelm Meru na kumpa maelekezo mbalimbali juu ya hatua iliyofikiwa kabla ya kiwanda hicho hakijaanza kufanya kazi na kuzalisha vifungashio.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt.Adelhelm Meru akiongea wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi katika kiwanda cha kutengeneza vifungashio cha Global Packaging Limited kilichopo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani ambapo alimpongeza muwekezaji wa kiwanda hicho na kutoa rai kwa wakuu wa wilaya na mikoa nchini kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya wawekezaji ikiwemo kutenga maeneo maalum kwa ajili ya viwanda kama ilivyo katika mkoa wa Pwani.
 Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt.Adelhelm Meru (katikati)akikata utepe kuashirika uwekaji wa jiwe la msingi katika kiwanda cha kutengeneza vifungashio cha Global Packaging kilichopo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani, wakwanza kushoto ni Mkurugenzi Muendeshaji wa Kiwanda hicho Bw. Joseph Wasonga, watatu kutoka kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Mlingi Mkucha akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Bi. Asumpta Mshana. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...