Na Evelyn Mkokoi-Singida

Wamilki wa Leseni za uchimaji mdogo wa madini wa Joshua Mine na Sekeknke one mine wa Sekenke Mkoani Singida, wametozwa faini ya shilingi milioni 10 kila moja kwa kosa la uchafuzi wa mazingira wa kutumia vibaya madini ya zebaki, hivyo kuhatarisha maisha ya viumbe hai.

Baraza la taifa la Hifadhi na usimamizi wa Mazingira limeitoza faini hiyo kupitia mratibuwa wa Barazakanda a Ziwa Bw. Jamali Baruti na kiwataka wamiliki hao kulipa faini hiyo ndani ya siku 14.

Adhabu hiyo inatokana na makelele katika eneo la uchimbaji, kusambaa kwa vumbi lisilovumilika, kukosekana kwa vyoo pia na matumizi mabaya ya miti katika uchimbaji wao ambao huenda sambamba na uharifu wa misitu.Aidha Baraza limewataka wachimbaji hao kuwa na vyeti vya tathmini ya athari ya mazingira pamoja na leseni ya uchimbaji.

Kwa Upande wake Mkuu wa Wiaya ya Mkalama Injinia Joakim Masakala akimuwaklisha mkuu wawiaya ya Iramba, alisema kuwa ni vizuri wakazi wa maeneo hayo wanavyojibidisha katika kazi lakini ni muhimu sana kuzingatia afya kwani uchimbaji wa kutumia madini aina ya zebaki bila vifaa salama kazini unaweza kuleta maradhi hususan ya saratani kwani madini hayo upenya kirahisi katika mwili wa binadamu.

Awali Katika Kikao na uongozi wa Mkoa pamoja na wadau wa Mazingira Naibu Waziri Mpina alitolea ufafanuzi masuala mbalimbali ya Mazingira ikiwemo matumizi ya Mifuko ya plastic na kuwashauri wakazi wa singida kutunza mazingira akitolea mfano wa ziwa Kitangiri lililoo Hatarini kutoweka kabisa. 

Katikati Bwana Jamal Baruti Mratibu wa Baraza la Taifa na Usimamizi wa Mazingira NEMC kanda ya ziwa, akitoa adhabu kwa wamiliki wa leseni za uchimbaji mdogo wa madini wa kampuni ya Jushua Mine na Sekenke one Mine wa Sekenke, mkoani Singida, kwa kosa la uharibifu wa mazingira kwa kutumia vibaya madini aina ya zebaki katika uchimbaji wao, pembeni yake ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akimsikiliza Bwana Baruti.
Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Rais Mungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akinyooshea kidole sehemu inayoonekana kuwa na maji katika ziwa Kitangiri Wilayani Iramba wakati kwa hali halisi ziwa hilo limepotea kabisa, hii ni kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi. 
Sehemu ya viongozi wa Mkoa wa Singida Pamoja na wadau , Wakimsikiliza Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina hayupo Pichani katika kikao cha pamoja cha kupokea ripoti ya Mazingira ya Mkoa na kutolea ufafanunuzi baadhi ya masuala ya swala zima la usimamizi wa mazingira nchini. (Picha na Evelyn Mkokoi OMR) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...