Na Benedict Liwenga-WHUSM.

WANAFUNZI wa kike wametakiwa kuongeza bidii katika masomo ya sayansi ili waweze kulisaidia Taifa katika kukabiliana na baadhi ya changamoto hususani katika sekta ya afya.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya wakati wa Mahafali ya Nne ya Shule ya Sekondari ya Wama Nakayama iliyopo Wilayani Rufiji Mkoani Pwani.

Katika Mahafali hayo, Mhe. Mhandisi Manyanya amewapongeza wahitimu wote na kuwaeleza kuwa, masomo yote yana umuhimu sawa lakini pale wapatapo fursa wasome kwa bidii masomo ya Sayansi kwani kwa sasa kuna changamoto mbalimbali zinazozikabili Taifa hususani katika sekta ya afya ambapo endapo mkazo ukitiliwa basi utasaidia kutatua baadhi ya changamoto hizo kama vile upungufu wa Wataalam wa masuala ya afya na hivyo kuweza kukabiliana na magonjwa mbalimbali.

Alisema kuwa, Serikali kwa sasa inajitahidi kuangalia maeneo yenye upungufu wa Wataalam mbalimbali ili iweze kutatua changamoto mbalimbali ambapo elimu bora inahitajika katika kuwapata wataalam watakaoweza kutatua mapungufu hayo ndiyo maana inajitahidi kutoa elimu bure kwa sasa na kuendelea kuhimiza wanafunzi kusoma kwa bidii hasa wasichana ili elimu itolewayo iwe sawa kwa wote pasipo ubaguzi na kuweza kumkomboa msichana.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya (kulia) ambaye alikuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akimkabidhi cheti mmoja wa Wahitimu wa Kidato cha Nne wakati wa Sherehe ya Mahafali ya Nne ya Kidato cha Nne Shule ya Sekondari Wama Nakayama iliyopo Wilayani Rufiji Mkoani Pwani 26 Novemba, 2016.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya (katikati) ambaye alikuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Shule, wageni waalikwa pamoja na Wahitimu wa Kidato cha Nne baada ya kumalizika Sherehe ya Mahafali ya Nne ya Kidato cha Nne Shule ya Sekondari Wama Nakayama iliyopo Wilayani Rufiji Mkoani Pwani 26 Novemba, 2016.

Mwenyekiti wa Shule ya Sekondari ya Wama Nakayama ambaye pia ni mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Salma Kikwete (kushoto) akimkabidhi zawadi mgenoi rasmi Mhe. Mhandisi Stella Manyanya wakati wa Sherehe ya Mahafali ya Nne ya Kidato cha Nne Shule ya Sekondari Wama Nakayama iliyopo Wilayani Rufiji Mkoani Pwani 26 Novemba, 2016.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...