Na Genofeva Matemu – WHUSM

Wazalishaji wa kazi za filamu nchini wametakiwa kuzalisha kazi zenye ubora na viwango vinavyotakiwa ili Tanzania iweze kupambana na mataifa mengine katika sekta ya filamu.

Rai hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo wakati wa ziara iliyofanywa na Bodi ya Filamu pamoja na makampuni mbalimbali ya watayarishaji Jana Jijini Dar es Salaam katika Studio ya Wanene Entertainment.

“Ili kuleta maendeleo chana ndani ya Sekta ya Filamu hatuna budi kuwa mabalozi wa tasnia hii kwa kuboresha ubora wa filamu zetu na kuweza kuliteka soko la ndani na nje ya nchi” alisema Bibi. Fissoo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Wanene Entartainment Bw. Darsh Pandit amesema kuwa kampuni ya Wanene imekubali kushirikiana na watayarishaji wa filamu za ndani ili kutoa filamu zenye ubora ambazo zitaleta mapinduzi kwenye tasnia ya filamu nchini.

Kwa upande wao watayarishaji wa ndani wa kazi za filamu wameliomba Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) kuanzisha kitengo maalum cha kutafsiri filamu za kitanzania ili ziwe na tafsiri inayoendana na kazi husika.

Wazalishaji wa filamu kutoka makampuni mbalimbali hapa nchini wametembelea studio hiyo ili kuweza kuangalia uwezekano wa kushirikiana katika kuzalisha filamu zenye ubora kupanua wigo wa tasnia ya filamu hapa nchini.

Baadhi ya Watayarishaji waliofanya ziara hiyo katika Studio za Wanene Entertainment ni pamoja na kampuni za Inspiration Image, Cut2cut Entertainment, 5 Effects, Steps na UWAFIMU.
Watayarishaji wa filamu kutoka makampuni mbalimbali wakiangalia moja ya kifaa kinachotumika kuandaa filamu katika Studio za Wanene Entertainment walipotembelea studio hizo katika kuboresha ubora wa filamu nchini Jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto waliokaa ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo.
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo akijaribu kupiga ngoma zinazotumika kuandaa kazi za muziki na filamu katika Studio ya Wanene Entertainment wakati wa ziara iliyofanywa na watayarishaji wa kazi za filamu kuboresha ubora wa filamu nchini Jana Jijini Dar es Salaam.
Watayarishaji wa filamu kutoka makampuni mbalimbali wakiangalia moja ya chumba kinachotumika kuandaa filamu katika Studio za Wanene Entertainment walipotembelea studio hizo katika kuboresha ubora wa filamu nchini Jana Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo.
Watayarishaji wa filamu kutoka makampuni mbalimbali, watendaji kutoka Bodi ya Filamu pamoja na watayarishaji kutoka Studio ya Wanene Entertainment katika picha ya pamoja wakati wa ziara iliyofanywa na watayarishaji hao katika Studio za Wanene Entertainment kuboresha ubora wa filamu nchini Jana Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...