AZIRI
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano la tatu la kitaifa la Afya
litakalofanyika Novemba 14 mwaka huu Jijini Dar es salaam.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Rais wa Kamati ya
maandalizi ya mkutano huo, Dkt. Omary Chillo wakati wa mkutano na
waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dar es salaam wenye lengo la
kujadili maendeleo ya sekta afya nchini.
Aidha
Dkt. Chillo alisema kuwa kongamano hilo litajadili jitihada ilizofikia
Tanzania katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo ya kimkakati ya
maisha yenye afya njema (SDG-3) yaliyokusudiwa kuifanya Tanzania kuwa
nchi ya wachapakazi.
Dkt.
Chillo aliongeza kuwa kongamano hilo pia linatarajia kujadili mikakati
ya kuboresha sheria ya usalama na afya makazini, kanuni na ufanyaji kazi
nchini kwa ajili ya maendeleo ya wafanyakazi na usalama wao.
Kwa
mujibu wa Dkt. Chillo alisema kuwa kongamano hilo pia linatarajiwa
kufanyika kuwakutanisha wataalam wa sekta ya afya 700 na kuratibiwa na
taasisi tano zikiwemo MoHCDGEC, TMHS,APHFTA,CSSC na BAKWATA.
Mkutano
huo ambao utakutanisha taasisi 53 za afya, zinatarajia pia kushiriki
katika maonesho ya bidhaa zinafanyika kwa ushirikiano wa Wizara ya Afya,
Maendeleo ya jamii, Jinsia , Wazee na Watoto pamoja na TAMISEMI tangu
kuanza kwake 2014.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...