Na Ally Daud-MAELEZO

AZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano la tatu la kitaifa la Afya litakalofanyika Novemba 14 mwaka huu Jijini Dar es salaam. 

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Rais wa Kamati ya maandalizi ya mkutano huo, Dkt. Omary Chillo wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dar es salaam wenye lengo la kujadili maendeleo ya sekta afya nchini. 

Aidha Dkt. Chillo alisema kuwa kongamano hilo litajadili jitihada ilizofikia Tanzania katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo ya kimkakati ya maisha yenye afya njema (SDG-3) yaliyokusudiwa kuifanya Tanzania kuwa nchi ya wachapakazi. 

Dkt. Chillo aliongeza kuwa kongamano hilo pia linatarajia kujadili mikakati ya kuboresha sheria ya usalama na afya makazini, kanuni na ufanyaji kazi nchini kwa ajili ya maendeleo ya wafanyakazi na usalama wao. 

Kwa mujibu wa Dkt. Chillo alisema kuwa kongamano hilo pia linatarajiwa kufanyika kuwakutanisha wataalam wa sekta ya afya 700 na kuratibiwa na taasisi tano zikiwemo MoHCDGEC, TMHS,APHFTA,CSSC na BAKWATA. 

Mkutano huo ambao utakutanisha taasisi 53 za afya, zinatarajia pia kushiriki katika maonesho ya bidhaa zinafanyika kwa ushirikiano wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia , Wazee na Watoto pamoja na TAMISEMI tangu kuanza kwake 2014.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...