Ujumbe kutoka kutoka jimbo la Eastern Cape kutoka nchini Afrika ya Kusini uko Nchini kwa ajili ya
kujifunza kutoka Tanzania namna bora ya fursa za kiuchumi kwa wanawake nchini, uwezeshaji wa
wanawake na uendeshaji wa Benki ya Wanawake Nchini.
Akiongea na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba
Nkinga kiongozi wa Msafara wa ujumbe toka Afrika Kusini Mhe. Nancy Sihiwaji Mbunge wa Jimbo la
Eastern Cape amesema ziara yaoa inatokana na utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa Wanawake
Afrika uliofanyika Nchini Afrika ya kusikini kuhusu uwezeshaji wanawake kiuchumi.
Aidha ujumbe huu umetambelea Wizara hii ili kujifunza na kupata uzoefu kutoka Nchini ni kuona ni jinsi
gani Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Njinsia, Wazee na Watoto
wameweza kuanzisha na kufungua Benki inayolenga kuwainua wanawake kiuchumi.
Mhe. Nancy Sihiwaji Mbunge wa Jimbo la Eastern Cape akimkabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga zawadi ya sikafu yenye ujumbe kutoka Jimbo la Eastern Cape leo ofisini kwake
jijini Dar es Salaam kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Jinsia kutoka Wizara hiyo Bw. Timoth Mgonja.
Mhe. Nancy Sihiwaji Mbunge wa Jimbo la Eastern Cape na ujumbe wake pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo
ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga wote katikati wakiwa katika picha ya pamoja leo walipomtembelea kwa
ziara ya mafunzo ya siku moja kupata uzoefu wa uwezeshaji wanawake kiuchumi hapa Nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...