Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.


BARAZA la wadhamini Simba limeweka msimamo wake wa kutokuutambua mkutano mkuu wa dharula uliotarajiwa kufanyika Desemba 11 na kuutaka uongozi wa klabu hiyo kuusimamisha mara moja mpaka pale madai ya wanachama yatakapovumbuliwa ikiwemo elimu kwa wanachama hao.

Taarifa hiyo iliyotolewa leo na Mwengekiti wa Baraza Mzee Hamis Kilomoni imesema kuwa baada ya kusoma nakala za barua za malalamiko zilizowafikia kutoka kwa baadhi ya wanachama wamekuta mambo mengi ya msingi huku wao kama ba

Ametaja baadhi ya mambo hayo, ni kuwa uongozi wa klabu ya Simba haujatoa elimu ya hisa kwa wanachama wake kama ilivyotakiwa, wanachama kuwekeana chuki miongoni mwao mpaka kufikia hatua ya kutukanana na kupigana ambapo mbali na hilo pia Uongozi wa Simba haukutoa taarifa za maboresho ya uendeshaji wa klabu kama mkutano mkuu wa Julai 31 ulivyotaka.

Kilomoni ameendelea na kusema, wao kama baraza la wadhamini na hawakuwa wameshirikishwa katika mchakato wowote wa mabadiliko ya uendeshaji wa klabu wamechukua hatua ya kuusimamisha mkutano huo mpaka pale uhakiki wa wanachama utakapofanyika kupitia kwa msajili wa vyama chini Baraza la Michezo Tanzania (BMT) kwani kwenye mkutano mkuu wa awali wengi waliingia na risiti na sio kadi, na kumtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kuusimamisha mkutano mkuu huo wenye kila dalili za uvunjifu wa amani huku kumbukumbu ikionesha kuwa Rais Evance Aveva alitolewa chini ya ulinzi mkali kwenge mkutano uliopita.

Baraza la wadhamini limewataka uongozi wa klabu ya Simba kutoa elimu kwa wanachama kama ilivyokuwa imekubaliwa kupitia matawi na mikutano ya wanachama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...