Timu ya Taifa ya mchezo wa kuogelea, imetamba kufanya vyema katika mashindano ya Dunia yaliyopangwa kuanza Desemba 6 mjini Windsor, Canada.

Tanzania itawakilishwa na jumla ya wogeleaji sita ambao wamepatikana kutokana na michujo mbalimbali ikiwa pamoja na mashindano ya Taifa yaliyofanyika mwezi Machi mwaka huu kwenye bwawa la kuogelea la Hopac.

Waogeleaji hao ni Hilal Hilal ambaye ni nahodha, Adil Bharma, Denis Mhini na Joseph Sumari ambao ni wanaume ambapo kwa wanawake ni pamoja na muogeleaji namba moja nchini, Sonia Tumiotto na Catherine Mason.

Akizungumza leo, Hilal alisema kuwa wamejiandaa vizuri chini ya kocha wao, John Belela na morali ipo juu kutokana na mafanikio waliyopata hivi karibuni katika mashindano ya kanda ya tatu yaliyofanyika Kigali, Rwanda na Tanzania kushika nafasi ya kwanza.

Hilal alisema kuwa lengo lao ni kupigia taifa lao na wanaamini watafanya vyema na hasa baada ya kuwaongeza wigo wa waogeleaji.

"Tumejiandaa kufanya vizuri, kama mjuavyo kwenye mashindano ya Afrika ya kanda ya tatu Tanzania ndiyo ilikuwa bingwa, tulipata medali 99, ushindani huu tutakwenda kuuendeleza Canada," alisema Hilal.
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Anastazia Wambura akikabidhi bendera kwa nahodha wa timu ya Taifa ya Kuogelea, Hilal Hemed Hilal.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...