Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.

JUMLA ya ajira 16,671 zimetengenezwa na viwanda vya uzalishaji nchini ambapo viwanda vya wawekezaji kutoka nje ya nchi vikiongoza kwa utoaji wa ajira hizo.

Takwimu hizo zimetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu ongezeko la wawekezaji nchini kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Waziri Mwijage amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inafanya juhudi za kuwahamasisha wawekezaji ili waweze kushiriki katika kuchochea mageuzi ya kiuchumi hivyo imeanza kupunguza uuzaji wa malighafi nje ya nchi ikiwa ni njia mojawapo ya kuwavutia wawekezaji kuwekeza nchini.

”Katika kujenga uchumi wa viwanda, tunalenga kujenga uchumi shirikishi na ulio endelevu ambao utahusisha watu wengi hivyo utaratibu wa aina hiyo utawasaidia kuwainua wananchi kiuchumi pamoja na kukuza pato la taifa,” alisema Mwijage.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage  akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu ongezeko la wawekezaji nchini katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...