Na Rhoda Ezekiel -Globu ya Jamii Kigoma,

MADIWANI wa Manispaa ya Kigoma Ujiji kupitia vikao vya kamati wamewasimamisha kazi watumishi wawili,ili kupisha uchunguzi wa upotevu wa takribani milioni 42 pamoja na matumizi mabaya ya fedha za miradi ya maendeleo kiasi cha shilingi milioni 250.

Maamuzi hayo yalichukuliwa mara baada ya kamati mbalimbali kujiridhisha na upotevu wa fedha kiasi cha milioni 42 ambazo zilihamishwa kutoka akaunti ya Amana na kupelekwa kwenye akaunti ya maendeleo na kutumiwa kulipa miradi mingine ya maendeleo iliyokuwa ikisimamiwa na Manispaa hiyo lakini pia matumizi mabaya ya fedha kiasi cha shilingi milioni 250 ambapo tume imeundwa ili kuchunguza zaidi tuhuma hizo.

Akitoa ufafanuzi Meya wa Manispaa hiyo Hussen Ruhava,mara baada ya maamuzi hayo alisema tume imeundwa kuchunguza watumishi wanne kati ya sita wamechukuliwa hatua za kinidhamu na kuwajibika kulipa fedha hizo huku kati ya hao wawili wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi na hatua za kisheria zitachukuliwa.

Ruhava aliiwataja walio simamishwa  kuwa ni Christina Nayingu ambae ni Mhasibu wa Manispaa na Michael  muhadhini wa Ndoliwa Muhadhina wasultani Ndoliwa na Dr Johni Tratra  kuwa watasimamishwa ili kupisha uchunguzi pindi utakapo kamilika,na  watatakiwa kulipa kiasi chote cha fedha kilicho tolewa.

Aidha Ruhava alisema licha ya maamuzi hayo lakini pia wameeleza kutokuwa na imani na Mkurugenzi wa Manispaa Judethadeus Mboya kutokana na kushindwa kukusanya mapato ipasavyo, asilimia kumi kutotolewa kwa vijana na wanawake, sanjari na asilimia 20 ya maendeleo kutokufika katika maeneo husika lakini pia sakata hilo lilimkumba na afisa mipango miji kushindwa kutekeleza maamuzi ya vikao vya madiwani na hivyo kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

" hatutaki kufanya maamuzi ya kumuonea mtu, hatutaki kuchukua maamuzi ya kuwa karibisha watu, tunacho hitaji watumishi wafanye kazi ya kuwatumikia wananchi bila ubadhilifu wowote na kutenda haki ",alisema Ruhava
 
MADIWANI wa Manispaa ya Kigoma Ujiji wakiendelea na vikao vya kamati ,ambapo wamewasimamisha kazi watumishi wawili,ili kupisha uchunguzi wa upotevu wa takribani milioni 42 pamoja na matumizi mabaya ya fedha za miradi ya maendeleo kiasi cha shilingi milioni 250.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...