Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
HISTORIA ya watumwa na kuanza kwa dini ya kikristo visiwani Zanzibar yawa kivutio kikubwa sana kwa watalii kutoka nchi mbalimbali kwa kufika katika Kanisa la The Cathedral Church of Christ lilijengwa na Bishop Edward Sterre kufahamu undani wakuja kwa dini hiyo kwneye visiwa hivyo.

Kanisa hilo limejengwa lilipokuwa Soko la watumwa lilijojengwa mwisho wa karne ya 19 pakitumika kama eneo la kuhifadhi watumwa wanaotolewa maeneo mbalimbali na Zanzibar ikiwa ndio kitivo cha biashara hiyo na Bishop Edward Sterre akaamua kuwanunua watumwa hao kwa lengo la kukomesha biashara ya utumwa na wakati wa ujenzi wa jengo la kanisa  watumwa walitumika kujenga na ikiwa ni kama  kuwakomboa na kisha baadae kuwabatiza na kuwa wakristo.

Kwa sasa kanisa hilo linaweza kupokea wageni kutoka mataifa mbalimbali  wanaoenda kufahamu historia ya watumwa na kuanza kwa dini ya kikristo pia kuna huweza kufika 1000 kwa siku kulingana na kipindi kilichopo.

Katika chumba kimoja cha watumwa walikaa takribani 75 yaani watoto 25 na wakubwa 50 na waliweza kukaa humo kwa kipindi kisichopungua siku mbili hadi tatu na wengine walikufa kutokana na kukosa hewa pamoja na kutokupewa chakula, mbali na hilo pia walifariki kwa magonjwa ya mlipuko kwani walikuwa wakilala juu ya kibaraza lakini kwa chini wakawa wanatumia kama sehemu ya haja ndogo na kubwa wakisubiri maji yajae baharini ili yaingie na kusafisha.

Picha za maeneo ya kanisa hilo liliopo eneo la Darajani Mkunazini Visiwani Zanzibar.
The Cathedral Church ambapo kabla ya kuwa kanisa lilitumika kama soko la watumwa visiwani humo wakiletwa kutoka sehemu tofauti kwa ajili ya biashara hiyo.
 Muonekano wa nje wa The Cathedral Church of Christ lilijengwa na Bishop Edward Sterre lililojengwa karne ya ya 19 kwa lengo la kukomesha biashara ya utumwa.

 Kanisa la Thed Cathedral Church of Christ katika muonekano wake wa ndani.
Wageni mbalimbali wakiwa wametembelea kanisa hilo na kufahamu historia ya watumwa iliyokuwa imeshamiri visiwani Zanzibar na kuanza kwa dini ya kikristo.
 Kinanda cha kwanza kutumika katika kanisa hilo na kinapatikana katika nchi kadhaa barani Afrika ikiwamo Visiwa vya Zanzibar.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...