Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde  amekabidhi vitanda vya hospital na vyandarua vyenye thamani ya Tsh 3,500,000 kwa Zahanat na vituo vya Afya 20 katika Jimbo la Dodoma Mjini.
Akiongea wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi vitanda hivyo,Mh Mavunde alisema amefanya hivyo ili kutatua changamoto ya ukosefu wa vitanda vya kutosha hali ambayo imekuwa ikisababisha usumbufu kwa wagonjwa wengi pindi inapotakiwa kupatiwa huduma kwa kupumzishwa katika zahanati hizo,Akaendelea kueleza kwamba Vitanda hivi vitasaidia sana kuboresha huduma ya Afya haswa katika maeneo ya pembezoni mwa Manispaa ya Dodoma na hivyo kuondoa usumbufu kwa wagonjwa pindi wanapohitajika kulazwa.
Wakati huo huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Ndg Kunambi amemshukuru Mbunge Mavunde kwa jitihada zake kubwa katika kuwahudumia wananchi wa Dodoma,na pia akaeleza kwamba tayari Manispaa ya Dodoma imeshaagiza magodoro kutoka MSD kwa ajili ya vitanda hivyo ili wananchi waanze kuvitumiq mara moja.

 Vitanda na vyandalua vikiwasili 
 Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde akikabidhi vyandarua kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Ndg Godwin Kunambi
 Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde akikabidhi vitanda kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Ndg Godwin Kunambi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...