Mrembo wa Miss Universe Tanzania 2017 Jihan Dimachk ameondoka leo alfajiri na ndege ya Oman Air kuelekea Manilla nchini Philipines kwa ajili ya kushiriki Mashindano ya Miss Universe. 

Jihan Dimachk aliyetwaa taji la Miss Universe Tanzania mapema mwezi Novemba mwaka jana anaenda kuiwakilisha Tanzania akiungana na wenzake kutoka nchi mbalimbali Ulimwenguni kuwania taji hilo. 

 Jihan Dimachk ameondoka akiwa amejiandaa vyema ikiwemo kisaikolojia, kimazoezi na kimavazi akishirikiana na wataalam mbalimbali kutoka hapa nchini. 

 Mkurugenzi wa kampuni ya Compass Communications  ambaye pia ndio Mkurugenzi na Muandaaji mkuu wa Kitaifa wa mashindano haya Maria Sarungi Tsehai amewashukuru wadau mbalimbali kwa kujitoa na kushiriki katika kuhakikisha mrembo wetu anatayarishwa vyema. 
 Mrembo wa Miss Universe akikabidhiwa bendera ya Taifa na Bi.Joyce Hagu akimwakilisha mkurugenzi wa kitengo cha sanaa.
 
 Miss Univere Tanzania Jihan Dimachk akiwa na Miss Universe Kenya Marry Esther Were uwanja wa ndege wa JK Nyerere wakati wakisubiri ndege kwa ajili ya kuanza safari.(katikati yao ni matron/mlezi wa Miss Universe Tanzania Happy Kimbe akiwatakia baraka za mwisho na ushindi mwema.)
Washiriki wa shindano la Miss Universe Tanzania wakimtakia kila la kheri kinara wao katika mwendelezo wa mshindano haya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...