Serikali mkoani Arusha imejipanga ndani ya kipindi cha miaka miwili iwe imekomesha migogoro ya ardhi sanjari na mivutano ya mikapa ya kiutawala kati ya wilaya moja na nyingine.

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo alisema hayo kwenye kikao cha Ardhi,Kilimo,Mifugo na Mazingira kilichowaleta pamoja wakuu wa wilaya,Wakurugenzi na Wenyeviti wa halmashauri pamoja na maafisa wengine kujadili kwa kina mbinu za kumaliza migogoro hiyo.

Alisema baada ya uhakiki wa mipaka na ushauri kutolewa eneo husika lipo Kijiji au wilaya fulani kiongozi au mwananchi atakayehamasisha uvunjifu wa amani atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Awali Mpima Ardhi mkoa wa Arusha,Hamdoun Mansoor akiwasilisha taarifa ya sekta ya ardhi alisema imekua ikitoa maelekezo ya kusimamia uendelezaji katika maeneo ya vijiji na miji kwa kuzingatia sheri ya ardhi namba 5 ya ardhi ya vijiji na 4 ya mwaka 1999 kanuni na taratibu zake.

Alisema changamoto inayoikabili sekta yake ni ujenzi holela unaofanyika kwa kasi kubwa katika maeneo ambayo kisheria yametangazwa kuwa maeneo ya Mpango,ambayo hayaruhusiwi kuendelezwa bila kupata kibali kutoka kwenye mamlaka husika.

"Serikali hujikuta ikilipa fidia zisizo za lazima wakati wa kuendeleza miundombinu mbalimbali na inapotaka kupeleka huduma nyingine za kijamii kwenye maeneo hayo,"alisema Manssor.

Aliyataja maeneo ya umma yanayopaswa kuhifadhiwa kuwa ni pamoja hifadhi za misitu,maeneo oevu,maeneo yenye vilima,vyanzo vya maji,mabonde na kingo za mito.

Manssor alisema uwezo mdogo wa halmashauri kulipa fidia umefanya maendeo mengi kutopangwa na kupimwa na hivyo kuruhusu ukuaji wa kasi wa makazi holela katika maeneo mengi ya mkoa na wilaya zake.

Migogoro ya mipaka ngazi ya mkoa ni katika vijiji vya Ngabobo, Olkung'wado, Leguruki, Ngejusosia, Miririnyi wilayani Arumeru mkoa wa Arusha na Kijiji cha Lekirimuni wilaya ya Siha mkoa wa Kilimanjaro ambayo inasababishwa na tofauti ya matangazo ya serikali namba 135 la mwaka 1954.
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akizungumza kwenye kikao cha kutatua migogoro ya Ardhi mkoani humo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...