Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
MGOMBEA wa Udiwani wa Kata ya Kijichi kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Tausi Milanzi amesema kuwa wananchi wamchague ili aweze kufanya kazi ya maendeleo ya Kijichi.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara wa Kampeni, Tausi amesema  yuko tayari kuwatumikia wananchi na sio jambo lingine hivyo anahitaji kura ndio itakayomuwezesha  kuwapa maendeleo.

Amesema vijana ndio wenye maamuzi hivyo watumie fursa ya kupiga kura ili aweze kushirikiana na vijana hao katika maendeleo.Tausi amesema kuwa yeye ni mwanamke mwenye uchungu wa maendeleo hivyo anaomba kura ndio aweze kutimiza malengo hayo.

Naye  Mbunge wa Mkuranga,na Katibu  Msaidizi  wa Kamati ya Wabunge wa  Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Ulega amesema wananchi wa kijichi wamchague Tausi kwa ajili ya maendeleo.
 Mgombea  wa Udiwani wa Kata ya Kijichi kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Tausi Milanzi akizungumza na wananchi wa kitongoji cha Sayari wakati wa kuomba kura leo.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.
 Kaimu Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam,Afidu Luambano akizungumza na wakazi  wa Kijichi wakati mkutano wa hadhara  wa  kuomba kura ya Mgombea wa Udiwani wa Kata ya Kijichi kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Tausi Milanzi leo katika mkutano wa hadhara wa kuomba kura.
 Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza wakati wa akimnadi Mgombea wa Udiwani wa Kata ya Kijichi kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Tausi Milanzi leo katika mkutano wa hadhara wa kuomba kura.
 Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akiwa ,amemshika mkono Mgombea wa Udiwani wa Kata ya Kijichi kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Tausi Milanzi leo katika mkutano wa hadhara wa kuomba kura.
 Mbunge wa Mbagala, Issa Mangungu akizungumza na wakazi  wa Kijichi wakati mkutano wa hadhara  wa  kuomba kura ya Mgombea wa Udiwani wa Kata ya Kijichi kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Tausi Milanzi leo katika mkutano wa hadhara wa kuomba kura.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...