WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amesema jumla ya vijiji 53 vya mkoa wa Njombe vitapatiwa
huduma ya maji safi na salama katika mwaka huu wa fedha.
Alitoa
kauli hiyo jana (Jumamosi, Januari 21, 2017) wakati akizungumza na wananchi wa wilaya
ya Wanging’ombe katika mkutano wa hadhara katika kata ya Ilembula.
Waziri
Mkuu alisema zaidi ya sh. bilioni 2.4 zimetengwa kwa ajili ya kugharamia mradi
huo wa maji katika miji ya Makambako, Njombe na wilaya ya Wanging’ombe.Alisema
kati ya vijiji hivyo vitakavyopatiwa maji, vijiji 22 ni vya wilaya ya
Wanging’ombe, hivyo aliwaomba wananchi hao kuwa na subira.
Kwa
mujibu wa Waziri Mkuu tayari zabuni ya mradi huo imeshatangazwa, hivyo
amewaagiza viongozi wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji watafute mkandarasi mzuri.Alisema
lengo la Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma
ya maji katika umbali usiozidi mita 400 kutoka mahali anapoishi.
Waziri
Mkuu alitoa kauli hiyo baada ya Mbunge wa Wanging’ombe, Mheshimiwa Mhandisi
Gerson Lwenge kumuomba awasaidie katika kutatua kero ya maji.Mbunge
huyo ambaye pia ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji alisema “Mheshimiwa Waziri
Mkuu sisi tunakabiliwa na changamoto ya maji, leo tunaomba ututatulie kero hii”.
Changamoto
nyingine aliyoitaja Mheshimiwa Lwenge ni pamoja na ukosefu wa hospitali ya
wilaya, ambapo Waziri Mkuu aliigiza halmashauri hiyo kuanza ujenzi.Alisema
Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 inaelekeza kuwa na hospitali katika
kila wilaya, kituo cha afya kwa kila kata na zahanati kwa kila kijiji.
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu
alimuagiza Mkuu wa Wilaya hiyo Bw. Ally Kasinge kukutana na viongozi wa kata na
vijiji vinavyozunguka hifadhi ya Mapanga Kipengele ili kutatua kero ya mpaka.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, JANUARI 22, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua jengo la Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe katika eneo la Igwachanya Januari 17, 2017. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe baada ya kuweka jiwe la msingi la jengo hilo katika eneo la Igwachanya , Januari 17, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea kiwanda cha chai cha Kibena wilayani Njombe Januari 21, 2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...