Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Laptop Mwandishi Chipukizi wa Vitabu vya Taaluma, Ali Salum Alujai ukiwa ni msaada aliompatia ili aweze kufanya vizuri zaidi katika uandishi wake. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Ikulu ndogo ya Njombe.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
MAJALIWA:SERIKALI IMEANZA KULIPA MADENI
YA WATUMISHI
*Jumla ya sh. bilioni 29 zililipwa
mwaka jana
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imelipa jumla ya sh. bilioni 29 kwa
watumishi mbalimbali wa umma wakiwemo walimu ikiwa ni sehemu ya madeni yao.
Alitoa
kauli hiyo jana (Jumamosi, Januari 21, 2017) wakati akizindua vyumba vitatu vya
kisasa vya madarasa katika shule ya sekondari Iwawa iliyoko wilayani Makete.
Waziri
Mkuu alisema Serikali imedhamiria kumaliza madeni ya watumishi hao, ambapo hadi
kufikia Novemba mwaka jana jumla sh. bilioni 29 zililipwa kwa watumishi 31,000.Alisema
kwa sasa Serikali imejipanga kuhakikisha hakuna madeni mapya yanayozalishwa
hivyo amewataka watumishi wa umma na wananchi kuendelea kuiunga mkono Serikali.
Hata
hivyo alisema Serikali inaendelea na mikakati ya kuboresha sekta ya elimu kwa
kujenga mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia.“Tumeanza
mradi wa ujenzi wa nyumba za walimu katika halmashauri nchini. Hapa Makete
tumeleta sh. milioni 557 kwa ajili ya ujenzi huo,” alisema.
Alisema
nyumba hizo za walimu zinazojengwa katika maeneo mbalimbali hususan ya vijijini
ni za kisasa ambazo zinalenga kuwaondolea changamoto ya makazi.Waziri
Mkuu alisema Serikali inafanya jitihada za dhati za kuhakikisha kila Mtanzania
anapata elimu kwa kuwa elimu ni kichocheo cha maendeleo ya jamii.
“Tumedhamiria
kumpatia elimu kila Mtanzania, hivyo halmashauri zihakikishe kila kijiji
kinakuwa na shule ya msingi na lazima ziwe na darasa la awali,” alisema.Naye
Mkuu wa Shule hiyo, Mwalimu Novatus Msivala aliishukuru Serikali kwa kugharamia
ujenzi wa vyumba hivyo vitatu vya madarasa na matundu 10 ya vyoo pamoja na uingizaji
wa maji kwenye vyoo na utengenezaji wa madawati 46.
Alisema
ujenzi huo umegharimu sh. milioni 95 ambao utasaidia kupunguza msongamano kwa
wanafunzi. Kwa sasa Serikali na wananchi wanaendelea kukamilisha ujenzi wa
vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya walimu.
Katika hatua nyingine jana Waziri Mkuu
alitimiza ahadi yake ya kumpatia laptop mwanafunzi Ally Alijai wa Chuo kikuu
cha SAUT tawi la Songea mkoani Ruvuma.Ahadi
hiyo aliitoa mwanzoni mwa mwezi huu alipokuwa katika ziara yake kikazi mkoani
Ruvuma, lengo likiwa ni kuendeleza kipaji cha utunzi wa vitabu kwa mwanafunzi
huyo.
Alisema
mwanafunzi huyo alionyesha umahiri mkubwa katika utungaji wa kitabu ambacho
kinaweza kutumika kufundishia katika shule za sekondari.
Hata
hivyo Waziri Mkuu alisema tayari kitabu hicho kimeshawasilishwa Taasisi ya
Elimu Tanzania (TEA) kuona kama kinaweza kuanza kutumika kwa kufundishia. Mwanafunzi
huyo alishukuru kwa zawadi hiyo na kuahidi kutunga vitabu vizuri zaidi.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, JANUARI 22, 2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...