Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu Yusuf Manji amefika katika kituo cha kati (Central Police) kwa ajili ya mahojino.Manji ambaye ni mwenyekiti wa klabu ya Yanga aliwasili majira ya saa 5 asubuhi akiongozana na mawakili wake.Baada ya kuwasili, Manji alisalimiana na wanachama wa klabu ua Yanga na kuingia moja kwa moja kituoni kuendelea na taratibu nyingine.
Mwenyekiti wa klabu ya Yanga ,Yusufu Manji akiwasili katika kituo cha Polisi Kati jijini Dar es Salaam mara baada ya kuamua kujipeleka hapo yeye mwenyewe kutii agizo la Mkuu wa Mkoa Paul Makonda,ambaye watuhumiwa wote 65 aliowataja jana katika sakata la dawa za kulevya,aliwataka kufika kesho Ijuma kituo cha Polisi kati kwa mahojiano zaidi.
Gari aliyowasili nayo Yusuf Manji.
Gari aliyowasili nayo Yusuf Manji.
Yusufu Manji akipokelewa na baadhi ya wanachama wa Yanga katika kituo cha Polisi kati mara baada ya kujipeleka leo badala ya kesho
Mnaji akiwa akiwa ameongozana na mawakili wake na wasaidizi kuingia kituo cha kati jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Yanga Yusufu Manji akisalimiana na Waandishi wa Habari jijini Dar ess Salaam katika kituo cha Polisi Kati.Picha na Hamphrey Shao- Globu ya Jamii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...