Hussein Makame, NEC-Bukoba
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevihimiza vyama vya siasa kutoa elimu ya mpiga kura kwa wapiga kura na wanachama wao bila ya kuegemea itikadi ya vyama vyao kwani sio wote wanaowaelimisha ni wanachama wao.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Emmanuel Kawishe wakati akitoa elimu ya mpiga kura kupitia kituo cha Redio Kasibante Fm kilichopo mjini Bukoba.
Alisema mdau namba moja wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni chama cha saisa na kwamba NEC inakutana na vyama hivyo mara kwa mara kushauriana namna ya kutoa elimu ya mpiga kura na namna ya kuwafikia wananchi wengi.
“Kwa hiyo Tume ya Taifa ya Uchaguzi inavihimiza vyama vya siasa kutoa elimu ya mpiga kura kwa wapiga kura na kwa wanachama wao pia” alisema Bw. Kawishe na kuongeza:
“Tena tunawasihi vyama vya siasa wasitoe elimu kwa njia ya itikadi za kichama watoe elimu isiyoegemea itikadi yoyote kwa sababu kuna wengine sio wanachama wa chama chake lakini watawapigia kura”
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Bukoba wakimsiliza Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Emmanuel Kawishe, wakati akitoa elimu ya mpiga kura.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...