Na Rhoda Ezekiel-Globu ya Jamii, Kigoma.

JESHI la Polisi Mkoani Kigoma limekamata Wahamiaji haramu 226, Kete za bangi 191, Heroin kete tano , pombe ya moshi lita 300 na silaha aina ya gobore moja, katika msako wa kupambana na dawa za kulevya, wahamiaji haramu pamoja na uhalifu uliofanyika kwa kipindi cha Wiki moja ili kuhakikisha Mkoa upo salama.

Akitoa taarifa ya Msako huo leo mbele ya Waandishi wa habari Mkoani humo , Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani Kigoma, DCP Fredinand Mtui alisema kuanzia Februal 2 mwaka huu jeshi la polisi Mkoani humo lilianza Msako wa kuhakikisha wanakomesha vitendo vya uhalifu, matumizi ya Dawa za kulevya na uuzaji pamoja na wahamiaji haramu wanaoingia Nchini bila vibali, hali inayo sababisha uhalifu kuongezeka kutokana na vitendo hivyo.

Mtui alisema kuwa mnamo februali 16 ulifanyika msako na kufanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu 203 katika kijiji cha Mganza Wilayani Kasulu wakitokea nchini Burundi wakiwa katika mashamba ya Wakulima,alisema na kuongeza kuwa Kigoma mjini walikamatwa wahamiaji 7 , kibondo 9 na Buhigwe 7a na jumla yao ni wahamiaji 226 ambao waliingia nchini Kinyume na utaratibu huku wakipokelewa na Wenyeji na wanawahifadhi.

Alisema Wengi wa wahamiaji hao wanatoroka Nchini mwao wakiwa wamefanya uhalifu na wanakuja Nchini na wanapokelewa na wenyeji na wanawatumia katika kilimo pia wengi wao ndio wanaotumika kifanya uhalifu mkoani humo ambapo Kamanda Mtui aliwaomba Wananchi kuacha kuwapokea Wahamiaji hao ambao wengi wao husababisha madhala makubwa katika maeneo yao.

Aidha Mtui alisema kwa upande wa madwa ya kulevya jeshi la polisi lilikamata katika Wilaya ya Kigoma kete za bhangi 191 sawa na gram10 pamoja na Heroin kete tano, Kasulu walikamata robo eka na gram 500 , kibondo miche 10 na Kakonko miche 60 ,kilo moja ya Bhangi madawa hayo yalikuwa yakiuzwa kwa vijana ambao wengi wao hawafanyi kazi na wanaendelea kufanya vitendo vya uhalifu.

" tumeweza kutoa kipaumbele katika uhalifu unao tusumbua kwa kiasi kikubwa Mkoani Kigoma ambao ni wahamiaji haramu , na matumizi ya Dawa za kulevya, kwa mujibu wa upelelezi tulio ufanya wengi wanaoingia bila vibali ni wale wahalifu wanao kimbia mikono ya sheria kutokana na uhalifu kama tunavyo fahamu muahalifu hawezi kuacha uhalifu kiurahisi ndio ambao wanakuja kiendelea kufanya uhalifu niwaombe Wananchi kuacha kupokea Wahamiaji halamu kwasababu kwa sasa tutakae mkamata anawahifadhi wahamiaji halamu watafikisha mahakamani", alisema Kamanda Mtui.

Alisema katika msako huo zilipatikana idadi ya kesi katika msako huo ni kesi ya uhamiaji haramu ni nane , kupatikana pombe ya moshi kesi 11, kupatikana Bhangi kesi tisa , kupatikana na silaha kesi moja na kupatikana na heroini kesi moja, watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani ilikuweza kujibu tuhuma zinazo wakabili.
Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani Kigoma, DCP Fredinand Mtui akizungumza na baadhi ya wandishi wa habari mapema leo kuhusiana na operesheni walioifanya ya kupambana na dawa za kulevya, wahamiaji halamu pamoja na uhalifu iliofanyika kwa kipindi cha Wiki moja ili kuhakikisha Mkoa upo salama.
Madumu ya pombe ya moshi (gongo),lita 300 zikiwa zimekamatwa
Kete za bangi 191 zikiwa zimekamatwa 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...