Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya
limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye tija katika maeneo
mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na limekuwa likishirikiana na
wananchi na wadau wengine katika jitihada hizo za kukabiliana na uhalifu na
wahalifu na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa matukio
makubwa ya uhalifu.
Kufuatia mapambano yanayoendelea nchi nzima dhidi ya watu wanaojihusisha na uuzaji na utumiaji wa dawa za kulevya, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanya misako na Mafanikio yaliyopatikana katika Misako ni kama ifuatavyo:-
Kufuatia mapambano yanayoendelea nchi nzima dhidi ya watu wanaojihusisha na uuzaji na utumiaji wa dawa za kulevya, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanya misako na Mafanikio yaliyopatikana katika Misako ni kama ifuatavyo:-
KUKAMATA WATUHUMIWA WANAOJIHUSISHA
NA BIASHARA YA UUZAJI/USAMBAZAJI WA DAWA ZA KULEVYA.
Mnamo tarehe 11.02.2017 majira ya saa 02:00 usiku, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilifanya misako
katika maeneo ya Manga na Nsalaga – Uyole na kukamata watuhumiwa wanaojihusisha
na biashara ya dawa za kulevya ikiwa ni pamoja na wauzaji, wasambazaji na
watumiaji [mateja]. Watuhumiwa waliokamatwa kutokana na kujihusisha ba
usambazaji na uuzaji wa dawa za kulevya ambao ni 1. SHABAN RAMADHAN [40]
Mkazi wa Uyole 2. RASHID YASIN [35]
Mkazi wa Nonde 3. RODA MWAMBERA [60]
Mkazi wa Mama John 4. MRISHO RAMADHAN
[22] Mkazi wa Airport - Iyela na 5. MUSSA KIMBE [33] Mkazi wa Nonde.
Watuhumiwa
wote wapo mahabusu na mahojiano zaidi yanaendelea ili kubaini mtandao mzima wa
watu wanaojihusisha na dawa za kulevya.
KUKAMATA WAUZAJI/WASAMBAZAJI WA DAWA
ZA KULEVYA.
Aidha
kufuatia misako iliyofanyika kuanzia
tarehe 19.01.2017 hadi tarehe 09.02.2017 katika maeneo mbalimbali Mkoani
Mbeya, Watuhumiwa wawili walikamatwa katika matukio mawili tofauti wakiwa na
dawa za kulevya.
Katika
msako wa kwanza uliofanyika maeneo ya Ilemi Jijini Mbeya, HENRY MWAMFUPE [19] Mkodishaji Baiskeli na Mkazi wa Ilemi
alikamatwa akiwa na kete 03 za dawa
za kulevya aina ya Heroine.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...