AFISA Ustawi wa Jamii Wilaya ya Wete Haroub Suleiman Hemed amewatumia zigo la lawama baadhi ya wakuu wa Taasisi na Idara za Serikali kwa akidai kwamba hawana mchango wowote katika kukabiliana na vitendo vya udhalilishaji .

Amesema baadhi ya wakuu hao wa Idara na Taasisi za Serikali wameshindwa kuonyesha nguvu zao katika kuunga mkono mapambano dhidi ya matendo hayo yanayoendelea kuiathiri jamii wakiwemo watoto wadogo .

Akizungumza kwenye kikao cha Maofisa wa Serikali ya Wilaya ya Wete , kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya , amesema wakuu hao wa Idara na Taasisi ni kikwazo kinachoviza mafanikio ya kuyatokomeza matendo hayo.

Ameeleza kwamba baadhi ya watumishi wa Serikali wanaokabiliwa na kesi ya udhalilishaji , hawahudhurii kikao wakiitwa huku hata wakuu wao wa taasisi hizo nao pia wameshindwa kushirikiana na Ofisi ya Ustawi wa Jamii kutafuta ufumbuzi wa masuala hayo.

“Baadhi ya wakuu wa Idara NA Taasisi za Serikali wanakuwa ni kikwazo katika kufanikisha mapambano dhidi ya matendo ya udhalilishaji , kwa kuwa wanashindwa kutoa ushirikiano wanapotakiwa kufanya hivyo ”alisema.
Na Masanja Mabula –Pemba

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...