Uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) umemalizika kwa mgombea Ahmad Ahmad kutoka nchini Madagascar kupata kura 34 dhidi ya 20 za aliyekuwa rais wa zamani Issa Hayatou uliofanyika leo nchini Ethiopia. 

Uchaguzi huo uliokuwa na ushindani mkubwa kutoka kwa pande zote uliweza kuhitimishwa na wanachama washiriki kutoka nchi mbalimbali barani Afrika kupiga kura za kumchagua ni nanai atakayeongoza shirikisho hilo kwa kipindi kijacho. 

Pamoja na uchaguzi huo, CAF wameweza kuipitisha Zanzibar kuwa mwanachama rasmi ambapo kwa sasa atakuwa mshiriki rasmi wa michuano ya kimataifa iliyo chini ya CAF pamoja na kuwa na timu ya Taifa inayojitegemea. 

Nchi takribani zote ziliweza kukubali kupatiwa kwa uanachama huo na nchi 51 kukubali na 3 kukataa ambazo ni Benini, Sychells na Madagascar.
Rais Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) Ahmad Ahmad kutoka nchini Madagascar

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...